ATMET: Tiba asili itajwe na katiba
BARAZA la Katiba la Chama cha Watabibu wa Tiba Asili
Tanzania (ATMET-Tanzania), limependekeza neno Tiba Asili litajwe katika Katiba
mpya.
Akizungumza kwenye mkutano wa majumuisho ya maoni ya Rasimu
ya katiba yaliyotolewa na Baraza hilo, wilayani Bagamoyo mkoani Pwani, Naibu Katibu wa ATME, Athumani Shem alisema
maoni hayo yatakabidhiwa kwenye Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Alisema pendekezo hilo ni miongoni mwa mapendekezo yaliyokusanywa
kutoka mikoa 25 na wilaya 133 za Tanzania Bara wakitambua kwamba Tiba Asili ni
taaluma kamili inayojitegemea kimuundo na kimaudhui ambayo ndiyo chanzo cha
tiba zote duniani.
“Huduma ya Tiba Asili ni huduma ya Afya hivyo kuna umuhimu
wa kutajwa kwenye katiba ya jamhuri ya muungano” alisema Shem na kuongeza kuwa
baada ya majumuisho hayo wangeyawasilisha na kuyabidhi maoni hayo ya waganga na
wakunga kwenye Tume ya mabadiliko ya Katiba hivi karibuni.
Akizungumzia changamoto hizo Shem, alisema ATME inakabiliwa
na ukosaji wa fursa kushiriki mikutano ya ndani na Kimataifa inayohusu huduma
za Afya, Tiba Asili, Tiba Mbadala, mapendekezo na maombi yao mbalimbali
kutopewa majibu kwa wakati
0 comments:
Post a Comment