Marekani yapata pigo Syria
DAMASCUS, Syria
HATUA Uingereza
kutangaza kujiondoa miongoni mwa nchi zitakazoshiriki katika kumsaidia Marekani
kwenye vita ya kuiondoa serikali ya Rais Bashar Al Assad.
Hatua hiyo inayoonekana
kuwa pigo kwa Marekani katika harakati zake za kuiondoa serikali ya Syria kijeshi
iliingia dosari jana baada ya bunge la nchini Uingereza kukataa jeshi lao
kuhusika na mzozo wa Syria.
Wazo hilo
lilikataliwa na bunge la nchi hiyo baada ya kukataa kupitisha mswaada uliokuwa
umepelekwa na Waziri Mkuu David Cameroon
ukiwashawishi wamuunge mkono waziri huyo kushiriki katika vita hivyo ili aweze kumsaidia
mshirika wake mkubwa Rais Barack Obama wa Marekani.
Wakizungumzia
kuhusu hatua hiyo wachambuzi wa siasa za Kimataifa wanasema kuwa uamuzi wa wabunge
wa Uingereza kukataa jeshi lao kuhusika na mzozo wa Syria ni pigo kwa Marekani ambayo
italazimika kwa sasa kutafuta uungwaji mkono kutoka kwa serikali ya Ufaransa
,Ujerumani na mataifa mengine makubwa.
Sababu ya wabunge wa Uingereza kuupinga mswada huo zinaelezwa
kuchangiwa na kuhofia matokeo ya baada ya uvamizi huo ambao utaendeleza mauaji
ya wananchi wa Syria na kusababisha mzozo huo kusambaa katika mataifa jirani
kama ilivyokuwa kwa nchi za Iraq na Libya.
Kauli kama hiyo pia imezungumzwa na waziri wa Ulinzi wa
Marekani Chuck Hagel aliyesema kuwa baada ya uamuzi huo wa bunge la Uingereza
kugoma kushiriki, Marekani itaendelea kutafuta uungwaji mkono kutoka kwa
mataifa mengine ili kuichukulia hatua serikali ya Syria kwa kutumia silaha za
kemikali dhidi ya raia wake.
Marekani imeituhumu Syria kwa kutumia silaha za kemikali kwa
kuwavamia raia wake wasiokuwa na hatia, na kuvunja sheria za kimataifa kuhusu
silaha hizo, tuhuma ambazo serikali ya rais Bashar Al Assad imeendelea kuzikanusha.
Nchi ya Ufaransa imeonekana kuunga mkono matumizi ya jeshi
nchini Syria baada ya Rais wan chi hiyo, Francois Hollande kunukuliwa akisema
kuwa kinachoendelea nchini humo hakikubaliki huku akishauri kutumia nguvu ya jeshi.
Rais Bashar Al Assad amesema kuwa tishio la Marekani la
kusema kwamba ikiwa uchunguzi utabaini silaha hizo zilitumiwa, italazimika
kuingilia mzozo huo kijeshi ni jambo ambalo halikubaliki kamwe na yuko tayari
kujilinda.
0 comments:
Post a Comment