Mahafali yatumika kupiga kampeini
MAHAFALI ya
darasa la saba katika shule ya msingi Saranga yamejikuta yakigeuzwa sehemu ya Kampeni
za kujinadi kwa Kamanda na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC),
Chris Kileo anayetajwa kutaka
kuwania jimbo la Ubungo kwa tiketi ya chama hicho katika uchaguzi ujao.
Tukio hilo
limetokea mwishoni mwa wiki, katika mahafali yaliyofanyika katika kata ya
Saranga, Kimara Temboni jijini Dar es Salaam.
Mgeni huyo alifika
akiwa amechelewa tofauti na ilivyotarajiwa na wenyeji wake ambao hata hivyo
walikata tamaa ya kumsubiri na nafasi yake kumkabidhi diwani wa kata ya Saranga,
Ephrahim Kinyafu (chadema) aliyekuwa mgeni mualikwa.
Wakiwa wanaendelea
na shughuli zao katika mahafali hiyo mara ghafla mjumbe huyo wa NEC, alifika
katika shule hiyo akiwa amevalia magwanda yanayovaliwa na makamanda wa chama
hicho akiongozana na walinzi watano waliokuwa wamevalia sare za Green guard.
Hali hiyo
ilizusha taharuki miongoni mwa wazazi na diwani Kinyafu aliyechukua uamuzi wa kuondoa
katika eneo hilo kwa maelezo kwamba alikuwa akiwahi shughuli nyingine.
Baada ya
kuondoka diwani huyo Tanzania Daima lilifanya mahojiano na diwani Kinyafu aliyeeleza
sababu za kuondoka kuwa ni kushindwa kuvumilia kukaa pale huku akiona sheria
zinavunjwa.
“Siwezi kuendelea kukaa katika eneo ambalo naona,
limevamiwa na watu wanaoeneza siasa mashuleni kinyume na taratibu za elimu,”
alisema Kinyafu.
Kutokana na
tukio hilo Tanzania Daima ilimtafuta Ofisa elimu wa Wilaya ya Kinondoni, Hussain
Ramadhani kwa njia ya simu ili kupata utaratibu wa tukio hilo aligoma
kulizungumzia na badala yake alisema tumtafute baadaye kwa sababu alikuwa kikaoni.
0 comments:
Post a Comment