“serikali isitishe tathmini
ya nyumba zate”
WAKAZI wa Mloganzila
wilayani Kisarawe mkoani Pwani, wameitaka serikali kuahirisha tathmini ya mali
zao hadi watakapoelezwa namna watakavyonufaika au athari zitajitokeza wakati
utakapotumika upana wa mita 10 au 22.5, kutoka barabarani hadi kwenye mali zao.
Katibu wa wanakikiji hao, Clara
Ibihya jana alieleza wasiwasi wao mbele ya Wakala wa Barabara (Tanroads), na Ofisa
wa Tathimini wa wilaya, kuwa unatokana na mazingira yaliyopo katika uendeshwaji
wake.
Alisema walichukua hatua
hiyo baada ya kubaini kuwa tathmini inayofanyika sasa haijajumuisha mali na
rasilimali zao kama vile mazao, majengo, ardhi na nyingine zilizoko ndani ya
upana wa barabara.
Ibihya aliongeza kuwa mvutano
huo unatokana wahusika wa mradi huo kutowashirikisha Wananchi kwa kupitia
viongozi wao kitendo kinachowapa wasiwasi kuwa huenda kazi hiyo ikawa imevamiwa
na walanguzi.
“Kutokana na malalamiko
yaliyotolewa na wanakijiji wenzangu tumekubaliana na wajumbe kuwa hoja kuu ya
mkutano huu iwe ni kukutana na wataalamu kutoka Tanroads kuhusu ufafanuzi wa
mradi wa barabara,”alisema.
Ibihya alisema wanakiji hao
walikubaliana kwa kauli moja kuwa fomu zote na picha zilizokuwa zimechukuliwa
awali kwa ajili ya kufanyiwa tathmini zirudishwe kwa ajili ya makubaliano
mengine.
“Tunataka zoezi la
tathimini lisitishwe mpaka hapo mamlaka husika itakapozungumza na Wananchi pia
fomu zitakazotumika katika kujaza taarifa zao itumike kwa lugha ya Kiswahili na
sio Kingereza,” alisema.
Alisema wakazi hao wanataka
mchakato huo lazima ufuate taratibu kwa kuwashirikisha viongozi wao wa Mkoa wa Pwani, kwa sababu tangu awali hawajashirikishwa hali inayowafanya wakose
utetezi.
Mhandisi wa Tanroads Chacha
Marwa, akiwa kwenye mkutano huo, alipotakiwa kutoa ufafanuzi kuhusu madai ya
wakazi hao alisema kipindi hicho alikuwa hakujiandaa kujibu maswali bali
alifika pale kwa ajili ya kufanya tathmini.
Naye mthamini wa Serikali
kutoka manispaa ya Temeke jijini Dar es Salaam, aliyetambulika kwa jina moja la
Moleka, aliwaeleza wakazi hao kuwa alikuwa hajui lolote bali alikwenda kule kwa
kazi moja ya kufanya tathmini.
0 comments:
Post a Comment