Social Icons

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sunday, September 29, 2013

Mtoto ang'atwa na mamaye sehemu za siri

WAKAZI wa Mlongazila wilayani Kisarawe mkoani Pwani wamelitaka jeshi la polisi kumkamata Moshi Hamad, kwa madai ya kumng’ata mwanaye wa kumzaa mwenye umri wa miaka sita, Khadija Hamad sehemu za siri, akidai amekuwa akijisaidia haja kubwa na ndogo hovyo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Tanzania Daima wilayani hapa juzi, wakazi hao, walisema mama huyo amekuwa na tabia ya kumfungia ndani mtoto wake huku akimchapa zaidi ya nusu saa jambo lililosababisha watoe taarifa kwenye dawati la haki za binadamu.
Walisema walifikia uamuzi huo baada ya kuchoshwa na vitendo hivyo ikiwemo kumpiga mwanaye huyo kwa kutumia nyaya za simu huku akimng’ata sehemu mbalimbali za mwili mtoto huyo na kumsababishia maumivu makali.
Stella Musa alisema sehemu za siri za mtoto huyo zimeharibiwa kutokana na kung’atwa na meno huku sehemu zake za  makalio zikiwa na vidonda ambavyo vinadaiwa  vimetokana na kuchomwa na  ncha kali.
“Wazazi wa mtoto huyo ni wanangu, siku moja mama wa mtoto huyo alishawahi kumuumiza mkono nilimchukua na kukaa naye nyumbani kwangu kwa mwezi mmoja nikimuhudumia kwa kumkanda kwa maji ya moto,”alisema Stela.
Mwalimu wa Shule ya Msingi Mlongazila ambaye ni katibu wa dawati la kutetea haki za binadamu Paulo Idana alisema suala hilo limewafikia hivyo wanachukua hatua za kisheria huku mtoto huyo amewekwa chini yao kwa ajili ya matibabu zaidi.
“Tulimfuata mama huyo Septemba 20 mwaka huu na tulifanya mahojiano mbele ya ofisa Mtendaji wa kijiji hiki na alikiri akisema alifanya hivyo kwa sababu ya  hasira lakini, sisi msimamo wetu tunafanya utaratibu ili tuweze kumfikisha kwenye vyombo vya sheria,”alisema Idana.
Akisimuliwa taarifa hiyo mtoto huyo, alisema wakati mwingine mama yake alikuwa akimwiita ili amfundishe kusoma na aliposhindwa aling’atwa mgongoni, mapajani na sehemu za siri huku akisema atafanyia hivyo hadi ajue kusoma ndipo ataacha kumwadhibu.
“Hivi vidonda vya mwilini mwangu ni vya kung’atwa wakati mwingine napigwa na waya, hiki kidole mama alinikata kutokana na kushindwa kusoma, alisema huku akilia kwa maumivu mtoto huyo.
Mama wa mtoto huyo, Moshi Hamad alisema alikuwa akitoa adhabu kwa mwanaye huyo  kutokana na kujisaidia haja ndogo na kubwa  hovyo wakati akirudi kutoka shule.
“Nafanya hivi kutokana na hasira siwezi nikamuona mtoto wangu anajisaidia haja kubwa na ndogo kwenye nguo nikamwacha tu lazima nimwadhibu mbona, kama jana alitapika kwenye sahani, je mtoto kama huyu nitamwacha,”alihoji Moshi.

Mwenyekiti wa Kitongoji hicho, Khadija Samizi alikiri kuwepo kwa tukio hilo hivyo serikali ya mtaa huo inafanya utaratibu ili kuhakikisha anafikishwa kwenye vyombo sheria.

0 comments:

 

Sample text

Sample Text

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sample Text