Social Icons

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Saturday, September 28, 2013

Kenya yajigamba kutoyumbishwa  na ugaidi

NAIROBI, Kenya
RAIS Uhuru Kenyatta wa nchini hapa, amesema kuwa nchi yake haitatishwa na vitendo vya ugaidi, wala shambulizi lililofanywa  hivi karibuni halitaivunja moyo serikali yake.
Akizungumza katika mkutano wake na wanahabari jijini jana, Rais Uhuru Kenyatta amewadhihaki magaidi waliohusika na shambulizi la West Gate kama waoga na wahalifu ambao njama yao ya kulitisha taifa na Wakenya imeshindwa.
Uhuru amewapongeza wakenya kwa kusimama pamoja na bila kujitenga na kukataa kutikishiwa na wahusika wa shambulizi la Westgate.Tamko hilo la Uhuru linakuja wakati ambapo waziri wa usalama wa Kenya Joseph Ole Lenku anasema wanawashikilia watu 8 wanaotuhumiwa kuhusika na shambulizi hilo la Westgate. Lenku amesema kati ya washukiwa 11, watatu walihojiwa na kuachiliwa.
Lenku ameongeza kuwa tayari wamewasiliana na polisi wa kimataifa Interpol kusaidia kuwasaka magaidi wa kimataifa akiwemo muingereza Samantha Lewthwaite.
Aidha Lenku ameongeza kuwa jumla ya watu 67 waliuawa kwenye shambulizi hilo wakiwemo maofisa sita wa usalama.
Pamoja na kutokea kwa tukio hilo lakini Kenya kwa kupitia waziri wake wa usalama wa ndani Joseph Ole Lenku, ameapa kutoondoa wanajeshi wake nchini Somalia.
Aliendelea kusema kuwa hawatafanya hivyo licha ya kuwepo kwa vitisho vya mashambulizi zaidi ya kundi la kigaidi la Al Shabab wiki moja baada ya shambulizi kubwa katika jengo la biashara la Westgate jijini Nairobi, lililogharimu maisha ya watu zaidi ya 67.
Waziri Lenku amewaambia waandishi wa habari kuwa hawatageuza mawazo kwa sababu walipeleka wanajeshi wao Somalia kwa kuwa kundi la Al Shabab lilikuwa tishio kwa usalama wa taifa la Kenya.
Alisema kwamba nchi yake itaendelea kuchukua hatua hadi hapo usalama na matakwa ya nchi hiyo yatakapolindwa.

Kauli hizo ni majibu kwa Mkuu wa kundi la Al Shabab nchini Somalia Ahmed Abdi Godane aliyesema kuwa shambulizi la Wastgate jijini Nairobi litafuatiwa na mashambulizi mengine ya umwagaji damu zaidi, mpaka hapo Kenya itakapoondoa wanajeshi wake nchini Somalia.

0 comments:

 

Sample text

Sample Text

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sample Text