Aliyeongoza mashambulizi balozi za
Marekani Kenya, Tanzania akamatwa
NEW
YORK, Marekani
MAJESHI
ya Marekani yamefanikiwa kumtia kizuizini Mshirika wa Alqaeda Abu Al Anas Al
Libi ambaye anahusishwa na kuongoza mashambulizi ya kigaidi ya mwaka 1998
katika balozi za Marekani nchini Kenya na Tanzania.
Hayo
yamethibitishwa na msemaji wa wizara ya ulinzi ya Pentagon ya nchini humo, George
Little akisema Libi ambaye jina lake
kamili ni Nazih Abdul Hamed Al-Raghie kwa sasa anashikiliwa kisheria na jeshi
la Marekani baada ya kufanyika kwa muendelezo wa operesheni za Marekani dhidi
ya ugaidi na kwa sasa yuko kizuizini katika eneo moja nje ya Libya.
Kiongozi
huyo wa kijeshi alikaririwa akizungumza katika kituo cha televisheni cha CNN
kuwa operesheni ya kumkamata mtuhumiwa Libi inakibali na inatambulika na
serikali ya Libya, ingawa vyombo vya usalama vya nchini Libya vimeeleza
kutotambua tukio lolote la kutekwa au kukamatwa kwa mtu huyo.
Serikali
ya Marekani ilitangaza donge nono la kitita cha dola za Marekani milioni 5 kwa
yoyote ambaye angemfichua alipo gaidi Libi anayetajwa katika orodha ya magaidi wanaowindwa
na nchi hiyo.
0 comments:
Post a Comment