Walimu Ilala wataka maelezo
madai yao
BAADHI ya walimu wa Shule
za msingi katika Manispaa ya Ilala jijini Dar es Salaam, wameutaka uongozi wa
wilaya kutoa maelelezo kuwa ni kwa nini wamekuwa wakicheleweshewa mshahara wao
kila mwisho wa mwezi unapofika.
Akizungumza kwa niaba ya
wenzake na Tanzania Daima jijini, kwa masharti ya kutoandikwa jina lake
gazetini, mwalimu huyo alisema wanaiomba Serikali Kuu kuiangalia hali hiyo
ambayo inaonekana kuota mizizi.
Mwalimu huyo alisema vitendo
hivyo vya kucheleweshewa mishara vimekuwa vikiendelea kwa mfano hadi sasa
mshahara wa Septemba hawajaupata.
Alisema wanashangaa kuona
kuwa wenzao wa Temeke na Kinondoni wamekuwa wakipokea mshahara kwa wakati kila
mwezi, lakini kwa upande wao sio hivyo.
“Sisi utaratibu huu wa
kucheleweshewa mishahara yetu unatukatisha tamaa kwa sababu kila wanapopitisha
siku wajue wanatujengea mazingira magumu ya kutoamini katika jamii tunayoishi
nayo huku mitaani kwani wengi wetu tunakopa tunauguliwa na wakati mwingine yote
hayo yanategemea mshahara mwisho wa mwezi”alisema mwalimu huyo huku akiungwa
mkono na wenzake.
Akizungumzia malalamiko
hayo, Ofisa habari wa Manispaa hiyo, Tabu Shaibu, alisema baada ya kupata
taarifa hizo, alifuatilia kwenye Idara ya Fedha ili kubaini tatizo liko wapi.
Alisema hata hivyo,
wahusika walimueleza kuwa mshahara ulikuwa umeingizwa kwenye Accounti zao za
Benki husika tangu Septemba 30.
“Kama kuna mwalimu ambaye
hajaingiziwa mshara wake, basi ni suala la yeye kufuatilia ili tatizo tulijue
na kulipatia ufumbuzi,”alisema Tabu.
0 comments:
Post a Comment