Wanigeria waandamana kupinga shirika
la Ufaransa
LAGOS,
Nigeria
MAMIA ya
raia nchini humo wamefanya maandamano kupinga kutekelezwa mapatano kati ya nchi
yao na Shirika la Kifaransa la Arva.
Maandamano
hayo yaliyowajumuisha wafanyakazi, wanafunzi wa vyuo vikuu, waandishi wa
habari, wanasiasa na viongozi wa taasisi zisizo za kiserikali, yalifanyika juzi
mbele ya bunge la Nigeria na karibu na ofisi ya shirika hilo la Ufaransa.
Waandamanaji
walishindwa kufika ofisi za Arva baada ya polisi kuweka uzio karibu na ofisi za
shirika hilo.
Mmoja wa
waratibu wa maandamano hao Ali Idris amesema “Kwa miaka 45 sasa Ufaransa
imekuwa ikishirikiana na viongozi wa Nigeria katika kupora madini ya uran ya
nchi yetu.”
Aidha mwanaharakati
huyo ameongeza kwa kusema kuwa, karibu taa 135 zimekuwa zikiwaka katika makazi
na makampuni ya wafaransa, zinawaka huku raia wa Nigeria wenyewe wakiendelea
kutumia kuni.
Amesema
kuwa, mikataba yote iliyowekwa kati ya serikali ya Abuja na Shirika la Arva la Ufaransa, haina usawa
wowote na miongoni mwa asilimia 70 ya madini ya urani yanayozalishwa nchini
Nigeria ni asilimia 5 pekee ya madini hayo ndiyo hubaki nchini humo.
Raia wa
Nigeria wanataka kubatilishwa mikataba hiyo kati ya serikali na shirika hilo.
0 comments:
Post a Comment