Social Icons

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sunday, December 22, 2013



Wanigeria waandamana kupinga shirika la Ufaransa

LAGOS, Nigeria
MAMIA ya raia nchini humo wamefanya maandamano kupinga kutekelezwa mapatano kati ya nchi yao na Shirika la Kifaransa la Arva.
Maandamano hayo yaliyowajumuisha wafanyakazi, wanafunzi wa vyuo vikuu, waandishi wa habari, wanasiasa na viongozi wa taasisi zisizo za kiserikali, yalifanyika juzi mbele ya bunge la Nigeria na karibu na ofisi ya shirika hilo la Ufaransa.
Waandamanaji walishindwa kufika ofisi za Arva baada ya polisi kuweka uzio karibu na ofisi za shirika hilo.
Mmoja wa waratibu wa maandamano hao Ali Idris amesema “Kwa miaka 45 sasa Ufaransa imekuwa ikishirikiana na viongozi wa Nigeria katika kupora madini ya uran ya nchi yetu.”
Aidha mwanaharakati huyo ameongeza kwa kusema kuwa, karibu taa 135 zimekuwa zikiwaka katika makazi na makampuni ya wafaransa, zinawaka huku raia wa Nigeria wenyewe wakiendelea kutumia kuni.
Amesema kuwa, mikataba yote iliyowekwa kati ya serikali ya Abuja na  Shirika la Arva la Ufaransa, haina usawa wowote na miongoni mwa asilimia 70 ya madini ya urani yanayozalishwa nchini Nigeria ni asilimia 5 pekee ya madini hayo ndiyo hubaki nchini humo.
Raia wa Nigeria wanataka kubatilishwa mikataba hiyo kati ya serikali na shirika hilo.

0 comments:

 

Sample text

Sample Text

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sample Text