Social Icons

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sunday, December 22, 2013



Chama tawala cha Gabon chashinda uchaguzi wa majimbo

LIBREVILLE, Gabon
CHAMA tawala cha Democratic(PDG), ambacho kimeongoza nchi hiyo kwa muda wa miaka 45, kimeshinda kwenye uchaguzi wa majimbo uliofanyika Desemba 14.
Akitangaza matokeo rasmi ya uchaguzi huo juzi, Waziri wa Mambo ya Ndani wa Gabon Jean Francois Ndongou amesema Madiwani 1,500 kati ya 2,404 wa Chama cha PDG wameshinda kwenye uchaguzi huo.
Chama hicho kimechukua majimbo 122, lakini kimepoteza majimbo ya Mouila, Bakoumba Oyem na Mitzic.
Matokeo hayo yanaweza kurekebishwa au kutenguliwa na mahakama ya katiba, ambayo ina uwezo wa kushughulikia mizozo ya uchaguzi.
Juzi asubuhi, Waziri Mkuu wa zamani Jean Eyeghe Ndong, ambaye chama chake cha Libreville kimechukua nafasi ya tatu, alisema yupo tayari kwa mazungumzo na chama tawala ili kuunda serikali ya muungano.

0 comments:

 

Sample text

Sample Text

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sample Text