Social Icons

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Thursday, August 29, 2013

40 wafariki ajali Kenya



NAIROBI, Kenya
TAKRIBANI watu 41 wameelezwa kuuawa baada ya basi moja la abiria lililokuwa likitoka Nairobi kuelekea Homabay Magharibi mwa Kenya kuanguka na kubingirikia mara kadhaa kabla ya kupata ajali eneo la Narok.
Taarifa kutoka kwa mkuu wa jeshi la polisi wilayani Narok Patterson Maelo imesema kuwa miongoni mwa waliokufa ni pamoja na watoto wanne huku dereva wa basi hilo alishindwa kulithibiti katika eneo la kona na hivyo basi hilo kupoteza mwelekeo na kuanguka.
Maofisa wa shirika la msalaba mwekundi ambao tayari wamefika katika eneo la tukio hilo wamesema kuwa watu wengine 33 waliojeruhiwa wamepelekwa hospitali ya wilaya ya Narok kwa matibabu.
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ni miongoni wa viongozi waliotuma risala zao za rambi rambi kwa jamaa na marafiki wa abiria waliouawa.
Katika ripoti iliyochapishwa kwenye mtandao wake wa twitter, rais Kenyatta ametoa amri kwa idara ya polisi kuchukua hatua dhidi ya wamiliki wa magari ya umma wanaokiuka sheria za barabarani.

BBC

0 comments:

 

Sample text

Sample Text

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sample Text