Social Icons

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Thursday, August 29, 2013

Mwanajeshi wa UN auawa na waasi DRC


KINSHASA, DRC
UMOJA wa Mataifa (UN), umesema kuwa mwanajeshi wake mmoja wa kutunza amani ameuawa na wengine watatu kujeruhiwa baada ya kutokea mapigano makali yaliyotokea Mashariki mwa nchini hapa kati ya wapiganaji na waasi.
Msemaji wa UN mjini New York, Farhan Haq ambaye hakutaja uraia wa wanajeshi waliouawa au kujeruhiwa alisema wanajeshi hao wa UN walitumia ndege za helkopta kuwasukuma nyuma wapiganaji wa M23 karibu na mji wa Goma, ambao ndio mji mkubwa zaidi katika eneo hilo la Mashariki.
Mapigano hayo yamekuwa ni mlolongo wa yale yaliyotokea mwaka 2012, baada ya waasi wa M23 kuuteka mji huo kwa muda kabla ya kuondoka kutokana na shinikizo kutoka kwa jamii ya kimataifa.
UN imetuma kikosi maalum cha kijeshi cha (MONUSCO) kinachoshirikiana na kile cha serikali  katika eneo hilo lenya utajiri mkubwa wa madini kukabiliana na waasi hao.
Jeshi hilo la Monusco limelazimika kufanya mashambulio ya anga na ardhini ili kuzuia waasi hao wa M23 kukaribia mji wa Goma na ripoti zinasema mapigano makali yanaendelea katika maeneo ya milima ya Kibati, takriban kilomita 15 Kaskazini mwa Goma.
Wapiganaji wa M23 wamesema kuwa wanajeshi wa Congo na wenzao wa UN walifanya mashambulizi ya anga na ardhini katika maeneo wanayoyadhibiti, Kaskazini mwa Goma.

BBC

0 comments:

 

Sample text

Sample Text

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sample Text