Social Icons

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Thursday, August 29, 2013

Kenneth: Deni la taifa ni maumivu kwa Wakenya

NAIROBI, Kenya
ALIYEKUWA mgombea wa nafasi ya urais, Peter Kenneth amesema kwamba kukua kwa deni la taifa ni mzigo kwa Wakenya iwapo halitatafutiwa ufumbuzi kwa makini.
Kenneth, alisema kwamba ukuaji wa deni hilo umekuwa kwa kasi ukilinganisha na ilivyokuwa mwaka 2008, ambako lilikuwa likifikia shilingi bilioni 700.
Alisema “Baada ya kupita miaka sita deni limekua na kufikia shilingi trilioni 2  na hali inavyoonesha deni hilo litafikia kiasi cha shilingi trilioni 2.5 hadi kufikia mwishoni mwa mwaka,”
Aliongeza kuwa “inawezekana miaka sita ijayo litafikia mara tatu, na hivyo kufanya asilimia 40 ya mapato kuelekea katika kulipa deni hilo,”.
Wakati wa kampeini za mwisho za uchaguzi mkuu wa nchini hapa, Kenneth alikuwa akitoa tahadhari ya hapo baadaye kukua kwa deni hilo la taifa.
Alisema kuwa kabla ya kumalizika kwa kauli yake hiyo sasa hali imeanza kujidhihirisha kwa deni la nchi hiyo kukua kwa kasi isivyo kawaida.

DailyNation

0 comments:

 

Sample text

Sample Text

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sample Text