Social Icons

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Friday, August 30, 2013

Kenya waanza kupambana





HALI ya sintofahamu katika kaunti ya Marsabit kaskazini mwa nchini Kenya imeendelea kuwepo baada ya watu 20 kuripotiwa kuuawa kutokana na mapigano ya kikabila yaliyotokea jana mchana.
Mapigano hayo yemetokea miongoni mwa kabila la Borana, Gabbra na Burji yanaelezwa kuchangiwa na mzozo wa ardhi na pia kuchochewa kisiasa.
Hata hivyo polisi wamepelekwa katika eneo hilo la Marsabit kuimarisha usalama na kwa sasa pole pole hali inasemekana kuendelea kurejea katika hali ya kawaida japo hofu kubwa bado imetanda miongoni mwa wakazi kutokana na kuzuka tena kwa mapigano.
Muda mfupi uliopita Amina Abubakar amezungumza na Sheikh Adan Wachu ambaye yuko katika kamati ya kutafuta amani katika eneo hilo, kwanza anaelezea hali halisi ilivyo katika eneo hilo kwa sasa.

0 comments:

 

Sample text

Sample Text

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sample Text