Social Icons

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Wednesday, August 28, 2013

Kingunge: Hakuna tija kuirudisha Tanganyika


MWANASIASA mkongwe nchini Kingunge Ngombale Mwilu amewashangaa baadhi ya watu wanaozungumzia urais wa Tanganyika kwenye mchakato wa katiba mpya huku wakishindwa kutafakari kutengeneza katiba itayomaliza tatizo la elimu na umasikini uliyokithiri nchini.
Mkongwe huyo aliyasema hayo Agosti 28, 2013 wakati alipokuwa akizungumza kwenye mkutano wa majumuisho ya maoni ya rasimu ya katiba ya Baraza la Chama cha matabibu wa Tiba Asili Tanzania (ATMET-Tanzania), Bagamoyo mkoani Pwani.
Kingunge alisema tangu kusomwa kwa rasimu hiyo hajasikia baadhi ya wanasiasa wakizungumzia umasikini unaowakabili Watanzania milioni 15 huku theluthi moja ya wananchi wote wakiwa hawajui kusoma.
Alisema mkoloni alipoondoka watu waliyokuwa hawajui  kusoma walikuwa asilimia 80, baadaye asilimia 90 wakawa wanajua kusoma lakini leo viongozi walioko madarakani hali katika sekta ya elimu ni mbaya na kufanya idadi ya watu wasiyojua kusoma inaongezeka kwa kasi.
Kingunge alisema wanapozungumzia katiba ina maana kwamba wananchi wanataka Katiba bora ili kuondoa upungufu lakini hadhani kama watafanikiwa kutokana na mpango wa wakubwa kujadili kurudisha majina ya nchi ambayo yalishafutika tangu mwaka 1964.
“Rasimu hii hazungumzii kuondoa matatizo yanayomkabili mwananchi masikini ambaye anaishi kwa mlo wa dola moja kwa siku haya ni matatizo makubwa”alisema.
Akizungumzia muungano Kingunge, alisema kuzungumzia serikali tatu ni sawa na kuanzisha mivutano, ambapo anaamini Tanganyika wakati huo lazima itataka kuwa zaidi ya serikali ya Muungano.
Aliongeza kuwa muungano huo umefanikiwa kwa kujenga umoja na kujenga utaifa ambao ni mfano kwa nchi za Afrika.
Kingunge aliongeza kuwa bado kuna umuhimu wake wa kuendelea kutumia fursa ya mabalaza ya katiba yakatumiwa kuamua Katiba mpya unayotafutwa uweje ambayo ni haki ya Watanzania.
Kwa upande wa Tuba asili aliwataka wataalami hao kuingeza kituhada katika kufanya tafiti ambazo zitasaudia kwa ajili ya kuisaidia serikali katuka sekta ya afya.
Alisema sio vyema wakabweteka wakisubiri hadi wapewe fedha na wazungu ndio wafanye utafiti kwa ajili ya kugindua tiba mbalimbali.

   

   

0 comments:

 

Sample text

Sample Text

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sample Text