RAIS
wa nchini hapa, amesema kuwa serikali yake imeshajiridhisha kwa taarifa za serikali
ya Syria kutumia silaha za kemikali kwa kuwavamia raia wasiokuwa na hatia
karibu na mji wa Damascus wiki iliyopita.
Obama
amesema kuwa matumizi ya silaha hizo zimeathiri maslahi ya taifa la Marekani na
huenda yakawa na matokeo mabaya kuhusu mgogoro huo wa Syria.
Hata
hivyo, rais Obama amesema kuwa hajaamua ikiwa jeshi lake litaivamia Syria
kijeshi siku moja baada ya azimio la Uingereza katika Baraza la Usalama la
Umoja wa Mataifa kutaka raia wa Syria kulindwa kushindwa.
Urusi
ambayo ni mshirika wa karibu wa Syria ilipinga azimio hilo na kusema kuwa
itaunga mkono azimio litakalosaidia kumaliza mzozo wa Syria Kidiplomasia na si
vita.
Katibu
Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon siku ya Jumatano alitoa wito kwa wajumbe
wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ambao ni nchi za Marekani, Ufaransa,
Uingereza, Urusi na China walioungana na kuzungumza kwa sauti moja ya kutafuta
njia ya kuiokoa Syria na kumaliza umwagaji damu.
Mpatanishi
wa Umoja wa Mataifa kuhusu mzozo huo wa Syria Lakhdar Brahimi, naye amesema
itakuwa sahihi kwa hatua za kijeshi kuchukuliwa dhidi ya Syria baada ya
kupitishwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Wachambuzi
wa siasa na usalama wanaona kuwa haitakuwa rahisi kwa azimio lolote linalolenga
kuishambulia Syria kupitishwa kutokana na Urusi na China ambazo ni washirika wa
karibu wa serikali ya Damascus.
Rais
Bashar Al Assad amesema kuwa tishio la Marekani kuwa ikiwa uchunguzi utabaini
kuwa silaha hizo zilitumiwa, italazimika kuingilia mzozo huo kijeshi ni jambo
ambalo halikubaliki kamwe.
Mwaka
uliopita, rais Obama alionya kuwa ikiwa serikali ya Syria itatumia silaha za
kemikali dhidi ya wapinzani, nchi yake itaivamia kijeshi.
Machafuko
nchini Syria yamesabisha zaidi ya watu 100,000 kupoteza maisha kwa kipindi cha
miaka miwili iliyopita kwa mujibu wa takwimu za UN na mamilioni kusalia kuwa
wakimbizi wakiwemo watoto.
REUTERS

0 comments:
Post a Comment