18 wauawa makabiliano na Boko Haram
TAKRIBANI watu
18 wamefariki kwenye makabiliano makali kati ya kundi la wapiganaji wa kiislamu
la Boko Haram na kundi la kijamii la kutoa ulinzi kwa raia, katika jimbo la
Borno Kaskazini Mashariki mwa Nigeria.
![]() |
| Vikosi vya Boko Haram |
Wengi wa
wale waliouawa waliaminika kuwa vijana wanaotoa ulinzi kwa wanavijiji waliokuwa
wanatoa ulinzi kwa mji wa Benisheik dhidi ya wapiganaji wa kiislamu.
Makabiliano
hayo yametokea siku chache baada ya jeshi kufanya mashambulizi dhidi kambi za
Boko Haram na kuwaua wanamgambo 50.
Boko Haram
linataka kuwepo kwa sheria za kiisilamu kote nchini Nigeria.
Kundi hilo
limekuwa likifanya mashambulizi mabaya tangu mwaka 2009, ambayo yamesababisha
vifo vya maelfu ya watu.
Lakini
mashambulizi ya aina hiyo yameongezeka zaidi katika siku za hivi karibuni licha
ya jeshi kupeleka wanajeshi wake katika maeneo yaliyoathirika zaidi.
Katika
kujibu ongezeko la mashambulizi yanayofanywa na kundi hilo Mei, Rais Goodluck
Jonathan alitangaza kuwepo kwa hali ya hatari katika majimbo matatu Kaskazini
mwa nchi hiyo likiwemo jimbo la Borno.
Jeshi
limeunga mkono ongezeko la makundi ya kutoa ulinzi katika majimbo hayo ili
kukabiliana na Boko Haram.

0 comments:
Post a Comment