Kerry: tunazidi kuungwa mkono
Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani John Kerry amesema idadi ya
nchi ambazo ziko tayari kuchukua hatua za kijeshi sasa imeongezeka mara
mbili,baada ya kufanya mazungumzo na mawaziri wa nje wa Umoja wa Ulaya huko
Lithuania.
Baada ya kufanyika kwa mkutano na mawaziri wa mambo ya kigeni wa
Umoja wa Ulaya, mawaziri hao wametoa wito kwa hatua kuchukuliwa dhidi ya rais
wa serikali ya Syria Bashar al Assad.
Marekani inaituhumu serikali ya Assad kwa kuwashambulia watu zaidi
ya 1400 kwa silaha za kemikali katika shambulio la Agosti 21 nje ya mji wa
Damascus.
0 comments:
Post a Comment