Assad akana
alitumia silaha za kemikali
RAIS Bashar
al Assad wa Syria amekanusha kuhusika na shambulio la silaha za kemikali mjini
Damascus mwezi uliopita.
Hayo aliyasema
wakati alipokuwa akihojiwa na televisheni ya Marekani, CBS ambako alieleza, ikiwa
serikali ya Rais Obama ina ushahidi kuwa alihusika, basi iutoe.
Rais Assad
aliongeza na kusema kwa kujihamini kuwa iwapo Marekani itafanya shambulizi
lolote washirika wa Syria watakuwa tayari kujibu shambulio lolote litalofanywa
dhidi yao.
Mwandishi wa
BBC mjini Washington anasema Rais Assad amechagua wakati muafaka kwa mahojiano
hayo, kwa sababu punde baraza la congress litaanza kujadili azimio kuidhinisha
Marekani kuchukua hatua ya kijeshi dhidi ya Syria.
Awali mwishoni
mwa wiki mjini Paris Waziri wa Mashauri ya Nchi za Nje wa Marekani, John Kerry,
alisema mawaziri wenzake wa Jumuiya ya Kiarabu walikubali kuwa ikiwa Syria
ilitumia silaha za kemikali, basi ilivuka mipaka ya viwango vya kimataifa.

0 comments:
Post a Comment