Ajali yaua watatu mkata
WATU watatu wamefariki dunia na
wengine watano kujeruhiwa katika ajali iliyotokea eneo la Mkata ikizihusisha
gari mbili ambazo ni Toyota Hiace na Roli.
Akizungumzia kuhusu tukio hilo
kondakta wa Hiace hiyo alisema kuwa ajali hiyo ilitokea kutokana na uzembe wa dereva
wake aliyekuwa anaendesha akiwa amelewa.
Kondakta huyo anasema kuwa
wakati walipofika katika makutano ya barabara ya kwenda Segera na Makata ndipo
dereva wake alishindwa kuiongoza gari yao na kujikuta akigongana uso kwa uso na
Scania hiyo ambayo ilikuwa ikmitokea Arusha na kwenda Dar es Salaam.
Majeruhi hao akiwamo dereva wa
Hiace aliyevunjika mikono yote wapo katika kituo cha afya cha Mkata kwa ajili
ya kupatiwa huduma ya kwanza.
0 comments:
Post a Comment