Social Icons

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sunday, September 1, 2013

Dabo: Nahitaji kutwaa tuzo nyingine

MSANII wa muziki wa kizazi kipya na mshindi wa Tuzo za muziki za Kilimanjaro nchini (KTMA), kwa upande wa ragga mwaka 2012-03, Predator Dabo amesema kwamba anatarajia kupata tuzo nyingine katika mashindano yajayo na kuendeleza rekodi yake.
Akizungumzia kuhusu namna atakavyohakikisha analinda heshima yake hiyo ya kupata tuzo nyingine msanii huyo amesema aliamua kukaa kimya pasipo kutoka kazi nyingine ili asome mchezo na kuachia ngoma kali ambapo kwa sasa ameachia kazi yake mpya inayokwenda kwa jina la ‘Niwe na wewe’.
Sababu za kuipatia nafasi ya juu ngoma hiyo na kuitabilia kufanya makubwa inachangiwa na kuitengeneza katika studio nzuri za One Love Fx chini ya mtayarishaji Tiddy Hotter.

Msanii huyo mwaka jana alipata tuzo hiyo akiwa ameingia kwenye kinyang’anyiro na wimbo unaojulikana kama ‘Ganja man’.

0 comments:

 

Sample text

Sample Text

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sample Text