Social Icons

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Friday, September 20, 2013

AU kujiondoa ICC

ADDIS ABABA, Ethiopia
VIONGOZI wa Afrika (AU), wanatarajiwa kukutana mwezi ujao mjini hapa, kujadili msimamo wa bara hilo kuhusu iwapo watajiunga na Kenya katika hoja ya kujiondoa kwenye Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC).
Mkutano huo unatarajiwa kufanyika kutokana na ombi la Kenya kutaka kikao cha dharura cha AU kujadili kesi zinazowakabili Rais Uhuru Kenyatta na naibu wake William Ruto.
Kuna taarifa zinaeleza kuwa ombi hilo la Kenya lina dalili za kuungwa mkono na mataifa mengi barani Afrika ambao wamekuwa wakiilalamikia mahakama hiyo kuegemea zaidi kwa viongozi wa bara hilo.
Tangu kuanza kwa kesi ya Makamu wa rais wa Kenya William Ruto, ICC wiki iliyopita, na ile ya Rais Kenyatta inayotarajiwa kuanza Novemba, dalili zimeonekana kuwa wengi hawana imani na mahakama hiyo wakiiona kama chombo cha nchi za Magharibi kukandamiza waafrika.
Kikao cha dharura kimeitishwa kujadili suala hilo baada ya Kenya kuonekana kutaka kuungwa mkono katika azma yake ya kujiondoa ICC.

Kuna uwezekano wa nchi wanachama wa mkataba wa Roma kujiondoa ICC lakini bado kuna nafasi ya maombi mengine kufanywa kuhusiana na hilo.

0 comments:

 

Sample text

Sample Text

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sample Text