Marekani
yataka UN iichukulie hatua Syria
WASHINGTON, Marekani
SERIKALI ya
Marekani imetoa wito kwa Umoja wa Mataifa (UN), kuja na azimio la kuichukulia
hatua serikali ya Syria kwa kosa lake la kutumia silaha za kemikali.
Marekani
imetoa wito huo kwa UN, Jana ikiutaka umoja huo kuichukulia hatua Syria kwenye
mkutano uliopangwa kufanyika wiki ijayo jijini New York.
Akizungumzia
hilo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani John Kerry amesema kuwa mgogoro wa Syria
umefikia katika hatua ya mvutano na kinachotakiwa ni UN kupitia baraza lake la
usalama kutekeleza kazi zake kwa vitendo.
Kerry alisema
kuwa muda wa malumbano umekwisha na kinachotakiwa ni kuhakikisha silaha za
kemikali zinaharibiwa huko Syria kwa kuwea tafsiri ya ripoti ya UN inaonyesha
kuwa serikali hiyo inahusika na matumizi ya silaha hizo.
Kiongozi
huyo amesema UN inawajibika kujiandaa kuchukua hatua kuhusiana na silaha hizo
za kemikali ambazo zimesababisha mauaji ya raia wasiokuwa na hatia.
Wakati
huohuo Rais Iran Hassan Rowhani amesema kuwa yuko tayari kuratibu mazungumzo ya
amani kati ya Serikali ya Syria na upinzani ili kumaliza mgogoro huo ambao
unaendelea kuiyumbisha Jumuiya ya kimataifa.
Rais Iran
Hassan Rowhan amesema kuwa nchi yake iko tayari kusuluhisha pande hizo ili
amani ipatikane nchini Syria kama njia ya kutekeleza sera ya Iran ya kujenga
badala ya kubomoa.
Serikali ya
Syria bado inashikilia msimamo wake kuwa haikutumia silaha za kemikali licha ya
kukubali kuziharibu ndani ya mwaka mmoja, silaha ambazo inazimiliki.
0 comments:
Post a Comment