Social Icons

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Wednesday, September 4, 2013

Garden Fc yang'ara Mama Kevin Cup

KOMBE la Mama Kevin limefikia tamati mwishoni mwa wiki kwa timu ya Garden FC ya Mtoni kwa Azizi Ali kutwaa ubingwa baada ya kuichapa timu ya Jiulize FC kutoka Tandika kwa mabao 2-0.
Katika fainali hizo zilizopigwa kwenye uwanja wa Sifa Mtoni, mtaa wa Sabasaba jijini Dar es salaam timu ya Galden FC iliyoibuka mshindi walikabidhiwa zawadi zao na Katibu wa Chadema Mkoa wa Temeke, Aloyce Waryoba.
Zawadi walizopewa ni kombe lenye thamani ya shilingi 550000,  jezi zenye thamani ya 250,000,  mpira wenye thamani ya shilingi 40,000 na mbuzi mwenye thamani ya shilingi 100,000 sambamba na fedha taslimu shilingi 100,000.
Wakati mshindi wa pili  Jiulize FC waliozawadiwa jezi zenye jezi zenye thamani ya 250,000,  mpira wenye thamani ya shilingi 40,000 na mbuzi mwenye thamani ya shilingi 100,000 sambamba na fedha taslimu shilingi 50,000.
Kwa upande wa mfungaji bora aliyefunga mabao saba, Juma Bahanuzi kutoka Jiulize FC aliyezawadiwa ngao ya kiatu cha dhahabu chenye thamani ya shilingi 100,000 sambamba na fedha shilingi 100,000.
Shindano hilo la soka lililodhaminiwa na Mwenyekiti wa Kata ya Chang’ombe kupitia chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Edith Bunjoro ‘maarufu kama mama Kelvin’ lililozinduliwa Julai 14 katika uwanja wa Chuo Kikuu cha ualimu (Duce) na Mbunge wa Ubungo, John Mnyika.
Katika uzinduzi huo Mnyika ambaye pia ni Mkurugenzi wa Mawasiliano wa CHADEMA) Taifa, alisema katika ilani ya uchaguzi ya CHADEMA 2010, ilikuwa ni suala walilokuwa wamelipatia kipaumbele.
Mashindano hayo yalishirikisha timu kutoka kata zote za Manispaa ya Temeke ambazo ni Senet  FC, Ubaya FC, Depo FC, Umoja FC, Scud, Panama, Masofa FC, Home Boy, Pama, Texas, Wajivuni, Wadude, Maji maji, Miduza, Jiulize na Dar United.
Katika shindano jingine la kuvuta kamba lililoshirikisha makundi mawili yote kutoka eneo la Mtoni washindi walikabidhiwa zawadi ya mbuzi mwenye thamani ya shilingi 100,000.
Pia kulikuwa na shindani la kufukuza kuku lililokuwa limewashirikisha wanachama wa Baraza la Wanawake Chadema wa kata ya Chang’ombe (BAWACHA) ambalo mshindi aliibuka kuwa Bishala Dausi aliyejishindia kuku mwenye thamani ya shilingi 20,000.

 Katika mashindano kama hayo ya kufukuza kuku lililoshirikisha akina mama wote wa Mtoni bila kujali itikadi za chama, Amina Saidi aliibuka kidedea kwa kujishindia kuku mwenye thamani ya shilingi 20,000.

0 comments:

 

Sample text

Sample Text

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sample Text