Putin:
Harakati za kijeshi Syria ni Uvamizi
DAMASCUS,
Syria
RAIS wa
Urusi Vladimir Putin, ameionya Marekani na nchi za Magharibi kuhusu hatua za
kijeshi wanazofikiria kuchukua dhidi ya Syria kuwa zitakuwa za kivamizi.
Alionya
kuhusu kuchukua hatua zozote za kijeshi dhidi ya Syria itakuwa ni uvamizi.
Kauli hiyo
imekuja hivi karibuni baada ya Rais wa Marekani Barack Obama kutoa wito wa
kuchukua hatua za kijeshi dhidi ya Syria baada ya kusema kuwa kuna uthibitisho
kuwa rais Assad ametumia silaha za kemikali dhidi ya wananchi wake.
Lakini
kwenye mahojiano na shirika la habari la Associated Press(AP), kabla ya mkutano
wa wiki hii wa G-20 mjini St Petersburg, Putin alisema kuwa huenda akaunga
mkono azimio la Umoja wa Mataifa (UN), ikiwa kuna thibitisho kuwa silaha za
kemikali zilitumiwa dhidi ya raia.
Putin
alipuuza wasiwasi kuwa wanariadha au mashabiki wataadhibiwa ikiwa watatoa matamshi
yatakayoonekana kuwa propaganda kuhusu mapenzi ya jinsia moja wakati wa michezo
ya olimpiki itakayofanyika nchini humo.
Wakati
huohuo, maseneta nchini Marekani wameridhia mswada wa azimio linalompa idhini
Rais Barack Obama kutekeleza shambulio la kijeshi dhidi ya Syria.
Pamoja na
kuriudhia lakini mswada huo unatarajiwa kupigiwa kura wiki ijayo.
Awali Waziri
wa mambo ya nchi za nje wa Marekani John Kerry alifika mbele ya Baraza la Seneti
ambapo alitoa onyo kwa maseneta wa Marekani kabla ya mdahalo wao kuhusu Syria
unaotarajiwa kufanyika wiki ijayo kwamba, hawapaswi kushindwa kutoa jibu la
kile alichokitaja kuwa ni matumizi ya silaha za kemikali ambayo hayawezi
kukanushwa yaliyofanywa na Rais Assad kwa watu wake mwenyewe.
Naye Katibu
mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amesema kuwa ikiwa itathibitishwa kwamba
silaha za sumu ya kemikali zilitumiwa nchini Syria, baraza la usalama la Umoja
wa Mataifa lazima liungane na kuchukua hatua.
0 comments:
Post a Comment