Social Icons

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Friday, September 27, 2013

H&B Agerup Foundation: WLF imeutendea haki mradi

TAASISI ya H&B Agerup Foundation ya nchini Marekani imeeleza kuridhishwa na utendaji mzuri unaofanywa na Taasisi ya nchini ya World Lung Foundation (WLF), katika mradi wake wa kuokoa vifo vya mama na mtoto.
Akizungumza juzi, Jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Taasisi ya H&B Agerup Foundation ambao ni wafadhili wakuu wa mradi huo, Dk. Helen Agerup aliimwagia sifa WLF baada ya kutoka katika ukaguzi wa mradi huo unaoendelea mkoani Kigoma.
Dk Agerup alisema kuwa “Nikiwa Kigoma nikikagua vituo tisa vya afya ambavyo vimo katika mradi wa WLF na nimeshuhudia wafanyakazi 26, waliopewa mafunzo ikiwamo na wananchi wa eneo hilo”.
Anaongeza kuwa akiwa katika mkoa huo alikutana wafanyakazi wa afya pamoja na viongozi wa Serikali na kubaini kwamba tangu mradi huo ulipoingia wajawazito wamekuwa wakihudhuria katika vituo vya afya ukilinganisha na hapo awali.
Alisema kuwa kabla ya mradi huo wajawazito waliokuwa wakihudhuria katika vituo vya afya kwa mwaka 2006 walikuwa 885, lakini baada ya kupata elimu kutoka WLF idadi hiyo imeongezeka mara dufu kwa Januari 2012 hadi Agosti 2013 wameongezeka na kuwa 1528”.
Dk. Agerup aliongeza kuwa katika kituo cha afya cha Ujiji kimeonesha mafanikio makubwa kwani mwaka 2007 wanawake waliokuwa wakihudhuria kituo cha afya walikuwa ni nane lakini mwaka jana walifikia 2,634.
Kutokana na mafanikio hayo Dk. Agerup aliahidi kuendelea kukufadhiri vituo vya afya na mradi kwa ujumla.
“Nawaahidi kushirikiana nao kwa karibu sambamba na serikali ya Tanzania nia ikiwa kupata matokeo chanya katika mradi huo wa afya ya mama na mtoto,” alisema Dk. Agerup.
Naye Mkurugenzi wa Mradi wa WLF, Dk. Nguke Mwakatundu alisema kuwa Taasisi hiyo imepanga kuongeza vituo vingine 10 vya afya katika miaka miwili ijayo ili viungane na vya sasa ambavyo ni 10.
Akielezea mafanikio ya mradi huo katika kuzuia vifo vya uzazi, Dk. Mwakatundu alisema kuwa kwa sasa wamefanikiwa ukilinganisha na mwaka 2006 -2011 ambako idadi yao ilikuwa 31 lakini baada ya mradi huo imepungua na kufikia watu watatu kwa miaka miwili ya 2012 -2013.

Dk. Mwakatundu alitoa wito kwa Serikali na asasi nyingine kuendeleza mradi huo katika mikoa mingine kama wao wanavyofanya kwa Kigoma.

0 comments:

 

Sample text

Sample Text

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sample Text