Social Icons

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sunday, September 8, 2013

Wanamgambo 50 Boko Haram wauwawa

JESHI nchini hapa limesema kuwa limewaua wanamgambo 50 wa kundi la Boko Haram kwenye operesheni iliyozinduliwa Kaskazini Mashariki mwa nchi hiyo katika kukabiliana na mashambulizi ya waasi, kwenye vurugu za karibuni kulikumba eneo hilo.
kikosi cha Boko haram
Taarifa kutoka kwa wakazi zinasema wanamgambo wanaoshukiwa kuwa wanatoka katika madhehebu ya kiislam yenye vurugu walifyatua risasi kwenye soko siku ya Alhamisi katika mji wa Gajiran, na kuua watu 15.
Msemaji wa jeshi Sagir Musa amewaambia waandishi wa habari mjini Maiduguri kwamba jeshi lilituma vikosi vya askari katika kukabiliana na azma ya washambuliaji ambapo kwa msaada wa vikosi vya anga waliweza kushambulia kambi za wanamgambo hao na kufanikiwa kuwaua 50

Mgogoro wa Boko Haram unakadiriwa kugharimu maisha ya zaidi ya watu 3,600 tangu mwaka 2009, ikiwa ni pamoja na mauaji yaliyotekelezwa na askari wa vikosi vya usalama, ambao wamekuwa wakituhumiwa kwa ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu.

0 comments:

 

Sample text

Sample Text

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sample Text