Mabasi ya haraka
yakalibia kuanza
MAGARI 366
yanatarajiwa kutumika katika mradi wa wakala wa usafiri wa haraka jijini Dar es
Salaam(DART).
Hayo yamebainishwa
jana na Kaimu Mtendaji Mkuu wa DART, Asteria Mlambo katika mkutano
uliowashirikisha DART na wamiliki wa Daladala wa jiji la Dar es Salaam.
Astela akifafanua
mpango kazi wa mabasi hayo, katika awamu ya kwanza ya mradi ambako alisema utatumia
mabasi makubwa 145 na mengine madogo 221.
Alisema makubwa
yatakuwa katika vituo vikubwa wakati madogo yatakuwa na kazi ya kuwatoa
wasafiri katika maeneo ya pembezoni mwa mji na kuwapeleka katika vituo vya
mabasi makubwa.
Aliwatoa hofu
wasafiri watakaokuwa wanatolewa pembeni na magari hayo madogo kuwa hawatalipa
nauli mara mbili.
Asteria
alisema ili wamiliki wa daladala wafaidi umiliki wa mradi huo wanatakiwa
kuanzisha kampuni mbili.
Alisema kuwa
miongoni mwa Kampuni hizo iwapo itaamua kuungana na nyingine ya nje yenye uzoefu
katika masuala ya usafiri kwa ajili ya kujipatia uzoefu huo haitazuiwa.
Akielezea faida
za kuanzishwa kwa Kampuni hizo alisema zitawawezesha kupata mikataba ya umiliki
wa mradi huo kwa kusimamia shughuli za ukatishaji wa Nauli ambazo zitakuwa katika
mfumo wa kadi kama zile zitumikazo benki ikiwamo na umiliki wa mabasi katika
mkatrabga utakaotumia miaka 12.
Alisema
“tunahitaji umiliki wa miradi hiyo iende mikononi mwa wamiliki wa daladala
ambao watapewa mabasi kwa kuchanganyiwa madogo na makubwa,”.
Faida
nyingine alisema ni kutoa kipaumbele kwa wamiliki wote wa daladala zinazotumia barabara
ya Morogoro kwa kuchangia mtaji wa mradi kwa njia ya hisa.
Kuhusu
wasiwasi wa suala la mapato, Mlambo aliwaeleza wamiliki hao kuwa mazingira
waliyotengeneza yatawawezesha kudhibiti mapato kwa kutumia tiketi za kadi
mithiri ya zile zinazotimiwa na benki.
Aliongeza
kuwa wataangalia malipo kulingana na kilomita ambazo gari itakuwa imekwenda hivyo
kusaidia wakati gari linapokuwa halijafanya shughuli kutotozwa.
Kuhusu
magari yaliyokuwa yakifanya shughuli zake katika barabara ambazo mradi huo unapita,
daladala zao zitatakiwa kupelekwa kufanya kazi katika barabara za nje ya mji.
Alitaja njia
kuu ambazo zitatumika katika mradi huo wa awamu ya kwanza ambao utatumia njia kuu
za Kimara hadi Kariakoo, Ubungo hadi Feri, Morroco hadi Kariakoo na Morocco
hadi Ubungo.
Naye Mkuu wa
Mkoa, Said Meck Sadik alisema kuwa amefarijika na mradi huo kwa sababu
utapunguza msongamano wa magari hivyo kusaidia watu kuwahi katika shughuli zao.
Meya wa jiji
la Dar es Salaam Dk. Didas Masaburi amesema kuwa watahakikisha mradi huo
unakuwa wa faida kwa kuepusha kutokea kama yale ya Shirika la Usafirishaji Dar
es Salaam (UDA) na mabasi mengine ya usafirishaji wa mkoani.
Akizungumzia
kuhusu magari hayo kama ni rafiki kwa walemavu alisema kuwa sehemu yake ya
kupanda ina wasaidia pia watu wenye ulemavu.
Masaburi
aliongeza kuwa katika mpango huo serikali haitakuwa na kazi ya kuhusika na
biashara na badala yake kubaki katika kuangalia miundombinu pekee.
0 comments:
Post a Comment