Social Icons

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sunday, September 1, 2013

Mandela atoka hospitali, arejea nyumbani

JOHANNESBURG, Afrika kusini
SERIKALI ya nchini Afrika Kusini imesema kuwa rais wa zamani wa nchini humo, Nelson Mandela (95), ametolewa hospitali leo alikokuwa akitibiwa mapafu tangu Juni.
Taarifa za kutolewa kwake hospitali na kurejea nyumbani zilitolewa kwenye tovuti ya Rais wa nchi hiyo zikieleza kuwa Mandela bado yu mahtuti na hali yake wakati mwingine inabadilika.
Lakini madaktari wake wanaamini akiwa nyumbani kwake mjini Johannesburg atapata matibabu sawa na yale ya hospitali.
Nyumba ya Mandela imebadilishwa ili kumruhusu kupata matibabu ya mgonjwa mahtuti akiwa nyumbani.
Serikali imesema inamtakia mema wakati akiendelea na matibabu.

0 comments:

 

Sample text

Sample Text

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sample Text