United kufunga dirisha dogo na Ozil?
KLABU ya Manchester United imeungana
na Arsenal katika kinyang’anyiro cha kumsainisha mchezaji wa Ujerumani anayekipiga
Real Madrid, Mesut Ozil na leo ikiwa ndio mwisho mwisho wa usajili wa dirisha
dogo.
Taarifa hizo zimetolewa na mtandao
wa Sky Sports ukisema imekuwa ikitapatapa baada ya kupokea kipigo cha 1-0 dhidi
ya Liverpool katika mechi iliyopigwa mwishoni mwa wiki hali iliyosababisha kocha
David Moyes kupigana kufa na kupona ili kumpata Ozil.
Arsenal, nayo imeonesha nia
ya kufanya kufuru katika kuhakikisha inamtwaa mchezaji huyo kwa usajili
utakaofikia kiasi cha Euro milioni 42.5.
Kocha wa Arsene Wenger alibainisha
mipango yake baada ya kumalizika kwa mechi yao ya jumapili waliyoibuka na ushindi
wa kupata bao 1-0 dhidi ya klabu ya Tottenham.
Alisema "tuymepanga
kufanya maajabu kwa mchezaji huyo katika saa 24 zijazo, ingawa ni uamuzi mgumu
lakini wa kushtua."
Ozil (24), alisaini kukipiga Real
akitokea Werder Bremen mwaka 2010 kwa dili la euro milioni 15 lakini amekuwa
akipambana kutafuta kucheza kikosi cha kwanza.
Ingawa taarifa kutoka Hispania
zinasema kuwa mchezaji Ozil hatakwenda kokote bali ataendelea kupigania namba chini
ya kocha Carlo Ancelotti.
Kwa nyongeza Ancelotti aliyekuwa
akifundisha Paris Saint-Germain anatarajia kuzungumzia suala la Ozil.
0 comments:
Post a Comment