250 wapoteza maisha Pakistan
ISLAMABAD,
Pakistan
WATU zaidi ya
250 wamepoteza maisha na wengine zaidi ya 300 kujeruhiwa baada ya kutokea kwa tetemeko
kubwa la ardhi lililopiga Kusini Magharibi mwa nchini humo.
Wakielezea
tetemeko hilo viongozi wa eneo hilo walisema limesababisha madhara makubwa kwa
wananchi ambao wengi hawana makazi baada ya nyumba zao kubomoka.
Serikali ya
Pakistan imeweka wazi kuwa inaendelea kuhakikisha inatoa msaada kwa waathirika
pamoja na kuchukua hatua kuhakikisha wanarejesha hali ya mambo kama
ilivyokuwapo hapo awali.
Serikali ya
jimbo la Balochistan imetangaza hali ya hatari katika wilaya ya Awaran ambayo
imeathiriwa zaidi na tetemeko hilo.
Kwa mujibu wa
mamlaka ya utabiri wa hali ya hewa ya nchi hiyo, tetemeko hilo linakadiriwa
kuwa nguvu ya 7.7 ukubwa wa richa.
Jeshi
limeendelea na harakati za uokoaji katika eneo hilo ambapo inahofiwa kuwa
huenda idadi ya vifo ikaongezeka zaidi kutokana na kuhofiwa kuwepo kwa wengine
ambao watakuwa wamefukiwa katika majengo yaliyoporomoka.
Makundi ya
wapiganaji waliojihami kwa silaha yameendelea kuwa changamoto katika wakati
huu, ambako juzi watu wenye silaha waliripotiwa kuwashambuliwa wahudumu wa afya
wanaowahudumia waathirika wa tetemeko hilo.
Tetemeko hilo
la ardhi limechangia kuharibiwa kwa huduma za mawasiliano na wasiwasi
umeendelea kutanda kwenye majiji mengine kama vile New Delhi na Dubai ambayo
yanahofia huenda yakakumbwa na tetemeko kama hilo.

0 comments:
Post a Comment