Iran, Marekani kupatana juu ya
nyuklia
TEHRAN, Iran
RAIS wa
Marekani Barack Obama na mwenzake wa Iran Hassan Rouhani kwa pamoja wameonesha
nia ya kutafuta suluhu ya kumaliza tofauti zao za kisiasa pamoja na mzozo
kuhusu mpango wa taifa hilo kuhusu Nyuklia.
Kwenye
hotuba yake kwa wajumbe wa mkutano wa 68 wa Umoja wa Mataifa (UN), Rais wa
Iran, Hassan Rouhani amesisitiza utayari wa nchi yake kuanza upya mazungumzo na
jumuiya ya kimataifa kuhusu mpango wake wa nyuklia licha ya kiongozi huyo
kutosema iwapo itaachana na mpango huo.
Rais Barack
Obama alipopata nafasi ya kuzungumza na wanahabari aliwaambia kuwa nchi yake
iko tayari kushirikiana na Iran na kwamba anamuagiza waziri wake wa mambo ya
kigeni John Kerry kuanza mazungumzo na viongozi wan chi hiyo.
Rais Obama
pia hakusita kuzungumzia mzozo uliopo kati ya nchi yake na Iran kihistoria
jambo ambalo anaamini ndilo limechangia kwa sehemu kubwa nchi ya Iran mara zote
kukataa kushirikiana nayo.
Katika hatua
nyingine waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amejibu hotuba ya rais wa
Iran, na kudai kuwa ni hotuba iliyojaa unafiki na ubinafsi kwa taifa la Iran
kwa kuwa rais Rouhan ameshindwa kusema iwapo atasitisha mpango wake wa
kutengeneza silaha za maangamizi.
Iran imekuwa
ikisisitiza kuwa mpango wake wa nyuklia ni halali na unazingatia haki za msingi
za kimataifa msimamo unaopingana na baraza la usalama la umoja wa mataifa
linalotaka Iran kuacha urutubishaji wa madini ya uranium.
Makubaliano
juu ya mpango huo yamekuwa yakigonga mwamba kwa muda mrefu lakini sasa Rais
mpya wa Iran ameonekana kuonyesha utayari wa kuafikiana juu ya suala hilo.
0 comments:
Post a Comment