Social Icons

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Thursday, September 5, 2013

Seseme: nitafanya mauaji Bilcanas

MSANII wa muziki wa kizazi kipya Seseme Haji ‘Spince Seseme’ amewataka mashabiki wake kuja kwa wingi kushuhudia shoo yake anayotarajia kuifanya katika ukumbi wa kimataifa Afrika Mashariki, Club Bilcanas siku ya jumapili.
Seseme anayetamba na kazi zake zinazokwenda kwa jina la ‘Ayaya’ na ‘Zinawauma’ amesema amepania kupiga shoo ambayo haitasahaulika kwa wapenzi wa burudani watakao hudhuria katika shoo hiyo.
Alisema kuwa ili kuhakikisha shoo yake inakuwa nzuri na ya kuvutia atahakikisha jukwaani anaingia kushambulia sambamba na wacheza shoo wake wake wanaocheza staili mbalimbali tofauti za kuvutia na za kisasa.

Seseme pia aliwaahidi mashabiki watakaofika hapo kuwaonjesha wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la ‘Sinderela’ utakaokuwa ‘surprise’ kwa rafiki yake mkubwa wanayeshirikiana naye katika kazi za muziki ambaye naye atamuweka hadharani kwa wale watakaohudhuria.

0 comments:

 

Sample text

Sample Text

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sample Text