Social Icons

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sunday, September 8, 2013

Uhuru Kenyatta ahakikisha serikali imara

RAIS wa nchini hapa, Uhuru Kenyatta amewahakikishia wakenya kuwa uongozi wa serikali yake utaendelea kuwahudumia wakenya, licha ya kuwa na kesi zinazomkabili na makamu wake William Ruto katika mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC) jijini Hague huko Uholanzi.
Kesi hiyo ambayo pia inamshirikisha mwanahabari Joshua Arap Sang inahusiana na vurugu zilizotkea baada ya uchaguzi wa mwaka 2007.
Rais Kenyatta amewataka wakenya kutokuwa na hofu kutokana na maneno ya watu wanaotaka kutumia nafasi hiyo kueneza uvumi kuwa Kenya haitakuwa na uongozi ikiwa rais Kenyatta na makamu wake watakapo elekea huko Hague badala yake amewaambia kuwa wao hawana hatia na anaamini watashinda na ushindi huo utakuwa wa wakenya.
Wakati hayo yakijiri jijini Nairobi huko Mombasa mdahalo kuhusu hatua ya wabunge wa Kenya kupitisha hoja ya kutaka taifa hilo kujitoa katika mkataba wa Roma uliobuni mahakama ya kimataifa ya ICC, bado unaendelea kupingwa na wananchi wakiwemo viongozi mbali wa kisiasa nchini humo.
Makamu wa zamani wa rais Kalonzo Musyoka amesema kuwa suala la kujiondoa katika mkataba wa Roma unaitangaza vibaya nchi hiyo kimataifa.
Rais Kenyata na makamu wake William Ruto wamepangiwa kuhudhuria baadhi ya vikao vya kesi zao kwa pamoja baadaye mwezi huu ambapo Ruto anatarajia kuondoka nchini Kenya leo kuelekea Hague Uholanzi ambapo rais Kenyatta atafuata baadaye.

0 comments:

 

Sample text

Sample Text

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sample Text