Social Icons

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Wednesday, September 4, 2013

Wafuasi wa Morsi wafungwa jela

CAIRO, Misri
WAKATI aliyekuwa rais wa nchini hapa, Mohammed Morsi akiwa katika kizuizi kisichojulikana akisubiri kufunguliwa mashtaka wafuasi wake watano wamefungwa kifungo cha muda mrefu jela.
Hukumu hiyo imetolewa na mahakama ya kijeshi ya Misri baada ya kuwapata na hatia ya kushambulia wanajeshi.
Mmoja wa wafungwa hao alifungwa jela maisha, wengine watatu wakipewa vifungo vya kati ya miaka 5, 15 na 45, kwa mujibu wa taarifa za jeshi.
Walishtakiwa kwa kosa la kuwafyatulia risasi wanajeshi wakati wa ghasia na vurugu katika mji wa bandarini ya Suez mwezi uliopita.
Vurugu hizo zilitokea baada ya msako mkali uliofanywa na maofisa wa usalama dhidi ya wafuasi wa Moris waliokuwa wamepiga kambi mjini Cairo.
Mamia ya wanachama waliofanya vurugu za Muslim Brotherhood, waliuawa wakati wafuasi wa Morsi walipokuwa wamepiga kambi nje ya msikiti wa Rabaa al-Adawiya na katika uwanja wa Nahda wakitaka Morsi aachiwe, ingawa waliondolewa kwenye kambi hizo Agosti 14.
Vurugu zilizotokea mjini Suez, Mashariki mwa Cairo, kati ya Agosti 14 na 16 zilisababisha vifo vya zaidi ya watu 30.
Hata hivyo haijulikani ikiwa wale waliohukumiwa Jumanne ni wanachama wa Brotherhood.
Lakini ikiwa ni wanachama wa Muslim Brotherhood, hukumu walizopewa bila shaka zitaathiri chama hicho hasa ikizingatiwa ni za kwanza kutolewa na chama hicho tangu kuondolewa mamlakani kwa Morsi.

Viongozi wa mashtaka walitangaza Septemba mosi, miezi miwili baada ya kuzuiliwa kwa Morsi kuwa anatufunguliwa mashtaka kwa kuchochea mauaji.

0 comments:

 

Sample text

Sample Text

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sample Text