AU: Kenyatta,
Bashir wasihudhurie kesi ICC
ADDIS ABABA,
Ethiopia
VIONGOZI
katika mkutano wa kilele wa Umoja wa Afrika (AU), wametaka kesi inayoendelea katika Mahakama ya
Kimataifa ya Uhalifu (ICC), dhidi ya Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta icheleweshwe
kwa ajili ya kutoa muda kwa kiongozi huyo kuendelea na majukumu ya kuwahudumia
wananchi wake.
Maamuzi hayo
yamefikiwa jana kwenye mkutano uliofanyika jijini hapa na kuwashirikisha
viongozi wa Afrika ambao wameishutumu mahakama ya ICC kuwa wamekuwa wakilenga zaidi
viongozi wa bara la Afrika katika kesi zake.
AU imeunga
mkono azimio linaloitaka ICC kutomshtaki kiongozi yeyote wa barani Afrika na
kufikishwa katika mahakama ya kimataifa ya Kimataifa wakati akiwa madarakani.
Mkutano huo
ulizungumzia pia suala la Afrika kufikiria kujiondoa kutoka ICC ambapo jambo
hilo halikuungwa mkono na wanachama wa kutosha.
Waziri wa
Mambo ya Nje wa Ethiopia ambaye ni mwenyekiti wa baraza kuu la AU, Tedros
Adhamom Ghebreyesus, amesema kuwa Umoja wa Afrika hauna mamlaka ya kumzuia
kiongozi wa taifa lolote kushtakiwa mjini The Hague ila jambo wanalofanya ni kuwasiliana
na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ili kulitaka kutoa idhini kwa kesi ya
Kenyatta kucheleweshwa kabla ya mashitaka yake kuanza rasmi Novemba 12.
Ghebreyesus
akizungumzia iwapo kama uamuzi huo hautachukuliwa basi viongozi wa Afrika watachukua
uamuzi wa kumzuia Kenyatta kuhudhuria katika mahakama hiyo mjini The Hague.
Alisema kuwa
uamuzi huo wa kutoshtakiwa kwa viongozi walioko madarakani hautaishia kwa Kenyatta
pekee bali hata kwa Rais wa Sudan Omar al-Bashir ambaye pia anatakiwa kufika hapo
kwa makosa ya uhalifu wa kivita.
Maamuzi hayo
yamepingwa na makundi ya kutetea haki za binaadamu, kutoka nchini Kenya ambako, Naibu
mkurugenzi mkuu wa Tume ya Kutetea Haki za Binadamu nchini Kenya (KHRC), Davis
Malombe alipinga wito huo wa AU wa kutaka kesi hiyo kucheleweshwe akisema “ni
jaribio jingine la kuvuruga na kuchelewesha haki kwa waathiriwa wa Kenya na
unasaliti madai ya ahadi ya AU ya kupambana na ukwepaji sheria”.
Baada
ya kuwasili mjini Addis Ababa, kabla ya kikao, Rais Kenyatta alitoa hotuba
iliyokuwa na maneno makali, akiishutumu ICC kuwa ni wakala wa himaya ya
kibeberu inayosambaratika.
Alisema
“Hata ingawa tuliongozwa na kudhibitiwa na mabeberu kwa maslahi ya kikoloni
katika miaka iliyopita, sasa hivi Afrika ni mataifa ya kijivunia na yaliyo na
uhuru. Zaidi ya yote, hatima yetu iko mikononi mwetu. Hivyo ni muhimu kwetu
kuwa macho dhidi ya mifumo inayoendelea kuwekwa na watu wa nje, wenye nia ya
kuidhibiti hatima yetu”.
Rais huyo wa
Kenya aliupongeza Umoja wa Afrika kwa kumuunga mkono huku akisema “Nikiwa kama Rais
wa Kenya, inanifanya nijivune kwa kuutegemea Umoja wa Afrika kwa kunisikiliza
na kunisaidia wakati wa matatizo hivyo naamini Afrika imesimama na mimi”.
Rais
Uhuru Kenyatta wa Kenya amesema kuwa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) si
chombo cha kutekeleza uadilifu bali ni mahakama ya kibaguzi na mwanasesere wa
madola ya kibeberu.
REUTERS

0 comments:
Post a Comment