Social Icons

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sunday, October 13, 2013

Wahamiaji haramu 50 wafariki bahari ya Mediterranean

MALTA, Italia
BOTI iliyokuwa imebeba wahamiaji haramu wanaokadiriwa kufikia 200 imezama katika bahari ya Mediterranean na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 50 katika kisiwa cha Malta vya nchini hapa.
Tukio hilo la boti kuzama limetokea umbali wa takribani kilometa 120 kutoka Lampedusa na takribani kilometa 110 kutoka visiwa vya Malta.
Serikali ya Malta na Italia wanashirikiana kufanikisha kazi ya uokoaji kwa kutumia helikopta na meli kwa ajili ya kuwabeba manusura wa ajali hiyo ili kuwafikisha katika eneo la nchi kavu.
Kwa mujibu wa takwimu za Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR), Italia ina wahamiaji haramu wanaofikia 32,000 ambao wamewasili Kusini mwa Italia na Malta kwa mwaka huu na tayari theluthi mbili wameomba kupewa uraia wa nchi hiyo.
Wahamiaji wengi zaidi waliowasili mwaka huu wamekuwa wakikimbia machafuko yanayoendelea nchini Syria na wengine wametokea katika mataifa ya Kaskazini mwa Africa.
Takwimu zaidi zinasema kuwa kuna zaidi ya wahamiaji 20,000 wamekufa maji katika kipindi cha miaka 20 iliyopita wakiwa katika harakati za kuingia barani Ulaya kwa lengo la kutafuta hifadhi na maisha bora.
Tukio hilo limetokea ikiwa ni wiki moja kupita baada ya boti nyingine iliyokuwa na wahamiaji haramu kutoka barani Afrika kuzama na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 300 karibu na visiwa vya Lampedusa Kusini mwa Italia.


0 comments:

 

Sample text

Sample Text

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sample Text