Social Icons

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Wednesday, October 9, 2013

Sudan: Juba iheshimu maamuzi ya AU

KHARTHOUM, Sudan
SERIKALI ya nchini hapa imemtaka jirani yake Sudan Kusini iheshimu na kufungamana na maazimio na maamuzi yaliyopitishwa na Umoja wa Afrika(AU).
Al-Khair Al-Fahim, Mwenyekiti wa Kamati ya Pamoja ya Usimamizi na Uongozi wa eneo la Abyei amesema kuwa, Sudan Kusini inapaswa kuheshimu maamuzi ya Umoja wa Afrika na isijichukulie maamuzi ya upande mmoja kuhusiana na kura ya maoni ya kuainisha hatima ya eneo la Abyei.
Hivi karibuni Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika liliitaka Sudan Kusini kutojichukulia maamuzi ya upande mmoja kuhusiana na kura ya maoni ya kuainisha hatima ya jimbo la Abyei.
Taarifa ya Baraza la Amani na Usalama la AU iliitaka Juba kushirikiana kikamilifu na Khartoum kuhusiana na suala hilo.
Sudan inaishutumu Sudan Kusini kwa kuitisha kura ya maoni kuhusu mustakbali wa eneo hilo mnamo Oktoba mwaka huu bila ya kuishirikisha Khartoum.

Eneo la Abyei linalozozaniwa na Sudan na Sudan Kusini ni jimbo lenye utajiri mkubwa wa mafuta ambalo liko katika mpaka wa nchi mbili.

0 comments:

 

Sample text

Sample Text

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sample Text