Social Icons

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sunday, October 20, 2013

Kenyatta: Nitahudhuria kesi ICC

NAIROBI, Kenya
RAIS wa nchini hapa, Uhuru Kenyatta amesema kwamba yuko tayari kuhudhuria kesi ya jinai inayomkabili katika Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC), Hague Uholanzi  baada ya mahakama hiyo kumruhusu kutohudhuria kwa baadhi ya vikao.
Akizungumzia hilo juzi, Rais Kenyatta aliishukuru ICC kwa kukubalina na uamuzi huo aliouona kama kujali maslahi ya Wakenya kwa kutoa muda kwa rais wao kuwaongoza badala ya kukaa kila kikao cha kesi yake huko Hague, hali itakayosababisha kukosekana muda wa kuwaongoza Wakenya.
Rais Kenyatta ameahidi kushirikiano na mahakama hiyo hadi mwisho wa kesi yake, kwa kuhudhuria baadhi ya vikao atakapokuwa akipata muda na kikao cha kwanza atakachohudhuria kitakuwa ni cha ufunguzi Novemba 12 na baadaye atarudi nchini Kenya.
Ingawa bado kuna taarifa zinaeleza kuwa itakuwa vigumu kwa Rais huyo kwenda Hague kutokana na viongozi wengi wa Kenya kuliona jambo hilo kama kumsababishia kiongozi wao kuonekana lege lege.

The Kenyan Daily Post

0 comments:

 

Sample text

Sample Text

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sample Text