Social Icons

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sunday, October 20, 2013

Majeshi ya Ujerumani yaondoka Kunduz

BERLIN, Ujerumani
VIKOSI vya jeshi la Ujerumani (Bundeswehr), vimeondolewa kutoka jimbo la Afghanistan la Kunduz baada ya kukaa kwa muda wa miaka 10 vikifanya operesheni ya kulinda usalama wa nchi hiyo.
Akizungumzia hatua hiyo juzi, Luteni kanali Heiko Diehl alisema kuwa wamefikiwa hatua hiyo ikiwa ni nia yao ya kuondoa majeshi ya NATO nchini humo baada ya kukamilika kwa opereshani yao.
Alisema kuwa “Tumekamilisha kwa mafanikio makubwa operesheni hii hivyo tumeona tujiondoe hasa baada ya kuwasili katika Mazar-i-Sharif na kuona hali ni shwari.
Kuondoka kwa vikosi hivyo vya Ujerumani kumepongezwa na kamanda wa eneo hilo wa jeshi la kimataifa linaloongozwa na NATO linalotoa msaada wa usalama kaskazini mwa Afghanistan, Meja jenerali Jörg Vollmer aliyejivunia mafanikio waliyofikia.
Alisema "Tunajivunia kile wanajeshi wetu walichofanikisha katika jimbo la Kunduz tangu walipo anza hadi walipofikia,"
Kabla ya kuondoka rasmi juzi jeshi la Ujerumani Bundeswehr lilikuwa limeshakabidhi kambi yao kwa jeshi la usalama la Afghanistan katika sherehe iliyofanyika Oktoba 6.

REUTERS

0 comments:

 

Sample text

Sample Text

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sample Text