Upinzani Guinea
wajiandaa kwenda mahakamani
GUINEA-BISSAU,
Guinea
WAPINZANI nchini
hapa wanatarajia kwenda mahakamani kupinga matokeo ya uchaguzi wa wabunge
yaliyotangazwa hivi karibuni ambayo yaliyokipa ushindi chama tawala cha RPG kinachoongozwa
na Rais wa nchi hiyo Alpha Conde.
Msemaji wa
muungano wa wapinzani Sydia Toure amesema kuwa kamwe hawawezi kutambua matokeo
ambayo hayawakilishi matakwa ya wananchi wa Taifa hilo.
Kauli
iliyoungwa mkono na mpinzani mkuu wa Rais Conde toka chama cha UDFG Cellou Dalein
Diallo aliyesema kuwa wana uthibitisho wa kutosha juu ya udanganyifu
uliofanyika katika uchaguzi huo.
Hatua hiyo
ya wapinzani imezusha hofu kuwa huenda machafuko yakalikumba Taifa hilo lenye
historia ya migogoro ya kisiasa na kijeshi na umwagaji damu kwa waandamanaji.
Mkuu wa
Umoja wa Taifa katika mataifa ya Magharibi mwa Afrika, Said Djinnit ametoa wito
kwa wapinzani kutafuta haki yao kwa kuzingatia misingi ya sheria na kuwa
watulivu wakati wakisubiri maamuzi ya mahakama juu ya uhalali wa matokeo hayo.
Msemaji wa
serikali Damantang Albert Camara amesema chama tawala kimeridhishwa na matokeo
hayo ambayo yamehitimisha mchakato huo uliochukua muda mrefu kumalizika.
Hata hivyo
waangalizi wa uchaguzi huo toka taasisi mbalimbali za kimataifa Oktoba 9, walisema
kulikuwa na dosari ngingi zinazoathiri uhalali wa matokeo ya uchaguzi huo.
Katika
matokeo yaliyotangazwa na tume ya uchaguzi siku ya ijumaa, chama tawala cha RPG
pamoja na vyama vingine shirika walipata jumla ya viti 70 kati ya 114 vya bunge
zima, ambapo RPG pekee ilipata viti 53 na washirika wake walipata 7.
Chama
pinzani cha UFDG kinachoongozwa na Cellou Dalein Diallo kilipata viti 37 wakati
chama cha Waziri Mkuu wa zamani nchini humo Sidya Toure cha UFR kilipata viti
10 na nafasi nyingine zilizobaki zilikwenda
kwa vyama vidogo vilivyoshiriki uchaguzi huo.
Matokeo hayo
yametangazwa ikiwa ni wiki tatu baada ya tukio la upigaji kura kufanyika, suala
ambalo lilizidisha hofu kuwa huenda udanganyifu unafanyika ili kukipa ushindi
chama tawala.

0 comments:
Post a Comment