Mwandishi ITV apigwa risasi
MTU mmoja anayedaiwa kuwa mchumba wa Ufoo Saro aliyefahamika
kwa jina la Ateri Mushi, amempiga risasi na kumjeruhi mwandishi wa habari wa
ITV, Ufoo Saro na kumuua mama mzazi wa mwandishi huyo, Anastazia Saro na kisha
kujipiga risasi mwenyewe.
Akizungumzia tukio hilo Kamanda wa polisi wa mkoa wa
kipolisi wa Kinondoni, Ruben Mchome alisema kuwa tukio hilo limetokea majira ya
alfajiri ya leo.
Alisema kuwa mwanaume aliyefanya mauaji hayo alikuwa
anafanya kazi katika Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) nchini Sudan kama ofisa
katika kikosi cha Sudan.
Kamanda Wambura amesema inasemekana kulikuwa kuna ugomvi
kati ya wawili hao ambapo walishindwa kuelewana na ndipo walipoamua kwenda kwa
mama mzazi wa Ufoo Saro.
Alipofika huko inadaiwa kuwa mwanaume huyo alimshutumu mama
mkwe wake kwamba anamtetea mwanaye yaani Ufoo Saro, ndipo mwanaume huyo
alipotoa bastola na kumpiga mama wa Ufoo Saro risasi kifuani na kumuua papo
hapo na kisha akampiga Ufoo Saro risasi ya mbili, moja ya tumboni na nyingine
mguuni.
Inaelezwa kuwa baada ya kudhani kwamba amewaua wote, ndipo
naye alipojifyatulia risasi kidevuni na kufariki dunia hapo hapo.
Nukuu nyingine kutoka kwenye mitandao jamii zinasema,
akizungumza kwa njia ya simu, Steven Chuwa wa ITV amesema tukio hilo limetokea
kwenye nyumba alikokuwa akiishi mama wa Ufoo Saro, Kimbamba nje kidogo ya jiji
la Dar es Salaam.
Imeelezwa kuwa Ufoo
alikimbizwa katika hospitali teule ya Tumbi (Kibaha) katika jitihada za kuuokoa
uhai wake na baadaye alihamishiwa kwenye hospitali ya Taifa ya Muhimbili katika
kitengo cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu (ICU).
Taarifa nyingine zinasema Mushi aliwasili nchini jana
na kufikia nyumbani kwa Ufoo alfajiri ya
leo na kisha wawili hao ndipo walipoondoka kuelekea nyumbani kwa mama mzazi wa
Ufoo ili kutafuta suluhu.
0 comments:
Post a Comment