Social Icons

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Thursday, October 31, 2013




Sakata la udukuzi, Marekani yaigeuka Ulaya
  

NEW YORK, Marekani
WAKUU wa ujasusi nchini hapa wamewageuzia kibao washirika wao wa Ulaya katika mgogoro unaohusu udukuzi wa mawasiliano ya simu, wakisema mashirika ya Ulaya ndiyo yaliyokusanya taarifa na kuwapatia wadukuzi wa Marekani.
Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Ujasusi (NSA), Keith Alexander na Mkurugenzi wa usalama wa taifa James Clapper wakati wakijibu maswali ya wabunge kuhusu mpango wa udukuzi wa Marekani.
Wakuu hao wa mashirika ya ujasusi ya Marekani waliyakanusha madai hayo kuwa ni ya uongo, kuhusu mashirika yao kunasa mawasiliano ya mamilioni ya simu, na kusema magazeti ya Ulaya yaliyochapisha madai hayo, hayakuelewa data walizokuwa wanazitumia kutoa madai hayo.
Maelezo hayo yamekuja wakati ofisa wa juu wa Marekani akisema Rais Barack Obama alikuwa akitafakari kuwapiga marufuku majasusi wa Marekani kunasa mawasiliano ya simu za viongozi wa mataifa washirika, kufuatia hasira za Ujerumani juu ya madai kwamba mawasiliano ya Kansela Angela Merkel yalidukuliwa.
Mkuu wa NSA, Jenerali Keith Alexander, na mkuruguenzi wa usalama wa taifa, James Clapper, walitoa ushahidi mbele ya bunge la Marekani na kusema kwamba msingi wa ripoti hizo ulikuwa kutolewa taarifa zilizokabidhiwa kwa magazeti ya Ulaya na Snowden.
“Madai ya waandishi wa habari wa gazeti la Le Monde la Ufaransa, El Mundo la Uhispania na L'Espresso la Italia kwamba NSA ilikusanya mamilioni ya taarifa za mawasiliano ya simu hazina ukweli wowote. Kwa kuweka mambo wazi kabisa, hizo siyo taarifa tulizozikusanya kuhusu raia wa Ulaya. Ni taarifa ambazo sisi pamoja na washirika wetu wa NATO tulizikusanya katika kuhakikisha usalama wa mataifa yetu na kusaidia operesheni zetu za kijeshi," alisema Jenerali.
Hayo yameibuka saa chache kabla ya jarida la Wall Street kulipoti kwamba uchunguzi wa kielektroniki ulifanywa na mashirika ya kijasusi ya Ufaransa na Uhispania nje ya mipaka ya mataifa yao, na wakati mwingine katika uwanja wa vita na kutoa taarifa zao kwa NSA.
Lilisema kuwa iwapo madai hayo yatakuwa kweli, yanaweza kuzifedhehesha serikali za mataifa ya Ulaya, ambazo zimeipinga kwa nguvu Marekani kwa madai ya kuwafanyia ujasusi raia wake.
Mwenyekiti wa Kamati ya Ujasusi ya bunge la Marekani, Dianne Feinstein, aliunga mkono utetezi wa wakuu hao wa ujasusi na kusema kuwa Marekani haikuzichunguza Ufaransa na Ujerumani, bali nchi hizo ndizo zilikuwa zinakusanya taarifa hizo, na kwamba Marekani ilikuwa inakusanya taarifa katika maeneo ya kivita ya NATO kama vile Afghanistan.
Wakati huo huo, maafisa wa ujasusi wa Ujerumani wanatarajiwa kukutana na wawakilishi wa mashirika ya ujasusi ya Marekani katika lkulu ya White House, kujadili madai ya ujasusi wa Marekani katika ujumbe utakao kuwa umewahusisha mshauri wa sera ya kigeni wa Kansela Merkel na mratibu wa idara ya ujasusi wa nchi hiyo.
Kwa upande wa Marekani, ujumbe wake unaowajumuisha mshauri mkuu wa usalama wa Rais Obama, Suzane Rice, mkurugenzi wa usalama wa taifa James Clapper na msaidizi wa rais wa usalama wa ndani na mapambano dhidi ya ugaidi, Lisa Monaco.

0 comments:

 

Sample text

Sample Text

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sample Text