Jeshi Kenya laua Al Shabab 30
NAIROBI,
Kenya
![]() |
| al Shabab kazini |
WANAMGAMBO 30
wa kundi la kigaidi la Al Shabab wameuawa nchini Somaia katika oparesheni ya
pamoja ya Jeshi la Kenya iliyoshirikisha askari wa serikali ya Somalia nje ya mji
wa Kolbiyo ulio katika mkoa wa Lower Jubba ulio karibu na mpaka wa Kenya na
Somalia.
Kwa mujibu
wa msemaji wa Jeshi la Ulinzi la Kenya (KDF)
Emmanuel Chirchir, oparesheni hiyo ya juzi ilichukua muda wa saa nzimana
kuua wanamgambo 30 wa Al Shabab.
Hatahivyo
msemaji wa Al Shabab amekanusha ripoti ya kuuawa wapiganaji wa kundi hilo na
badala yake amedai kuwa wamewaua
wanajeshi wanne wa upande wa pili katika
mapigano hayo.
Mji wa
Kolbiyo umekuwa ukitumiwa na wanamgambo wa Al Shabab kutekeleza mashambulizi
ndani ya ardhi ya nchi ya Kenya kwa muda wakiitaka Kenya kuondoa vikosi vyao
nchini humo.
Alhamisi
Jeshi la Ulinzi la Kenya lilitangaza kuwa lilitekeleza shambulizi la angani
ndani ya Somalia na kuharibu kambi ya mafunzo ya wanamgambo wa al Shabab
waliohusika na hujuma dhidi ya jengo la maduka la Westgate mjini Nairobi Septemba
mwaka huu.
KDF imemtoa
taarifa iliyosema kuwa kambi hiyo ilikuwa na wapiganaji 300 ambao baadhi
waliwaua na wengine kujeruhiwa.

0 comments:
Post a Comment