Social Icons

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sunday, October 20, 2013

Republican kumpinga Obama kuhusu Iran

WASHINGTONG, Marekani
MASENETA kadhaa wa chama cha Republican katika Congress ya Marekani wamesema watawasilisha muswada wa kuiwekea vikwazo zaidi Iran kufuatia ripoti kuwa serikali ya Rais Barack Obama inafikiria pendekezo la kuirejeshea Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mali zake zenye thamani ya mabilioni ya dola zilizokuwa zimezuiliwa na Washington.
Hayo yameelezwa na gazeti la New York Times liliripoti kuwa serikali ya Marekani inapanga kuzirejesha mali za Iran kama hatua ya kuifanya Tehran nayo ichukue hatua ya kuwa na imani na serikali ya Washington katika uhusiano wao wanaotaraji kuuanzisha kuhusu miradi ya Iran ya nyuklia.
Hata hivyo Maseneta Lindsey Graham, Kelly Ayotte na Mark Kirk kutoka chama cha Republican wametoa taarifa wakitaka serikali ya Obama iiwekee vikwazo zaidi Iran.
Baada ya mazungumzo ya Geneva, serikali ya Marekani ilisema kuwa mazungumzo hayo ya nyuklia kati ya Iran na kundi la 5+1 yaliyofanyika Oktoba 15 na 16 yalitoa mwanga wa matumaini.
Inafaa kukumbusha hapa kuwa Marekani na Umoja wa Ulaya zimeiwekea vikwazo vya uchumi vya upande mmoja Iran kwa kutumia kisingizio cha tuhuma zisizo na ushahidi kwamba Tehran ina nia ya kuunda silaha za nyuklia madai ambayo yamekanushwa mara kadhaa na Jamhuri ya Kiislamu

0 comments:

 

Sample text

Sample Text

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sample Text