Vyama vya
Tunisia vyashindwa kumteua waziri mkuu
TUNIS,
Tunisia
CHAMA tawala
nchini hapa, Ennahda pamoja na vyama vingine vya upinzani vimeshindwa kufikia
muafaka kuhusu nanai anastahili kuwa waziri mkuu mpya wa nchi hiyo.
Kushindwa huko
kukubaliana kumechangiwa na pande zote mbili zilizokuwa zimekaa kikao cha
faragha mwishoni mwa wiki mjini Tunis lakini hakuna mapatano yaliyofikiwa.
Kuna mvutano
kuhusu vigogo wawili, Mohammad Ennaceur (79), anayeungwa mkono na upinzani na
Ahmad Mestiri mwenye umri wa miaka 88 ambaye anaungwa mkono na Ennahda.
Atakaye
chaguliwa kuwa waziri mkuu atakuwa na jukumu la kuunda serikali ya muda ambayo
inapaswa kuwa na watu wasiopendelea upande wowote ili kuitayarisha nchi hiyo
kwa ajili ya uchaguzi mkuu.
Tunisia
ilitumbukia katika machafuko mwaka 2011 baada ya kuondolewa kwa utawala wa dikteta
wa zamani Zine El Abidine Ben Ali kufuatia mwamko wa wananchi.
Mgogoro wa
kisiasa ulipamba moto Tunisia baada ya kuuawa mwanasiasa mwandamizi wa upinzani
nchini humo Julai mwaka huu.
0 comments:
Post a Comment