Wanahabari
wawili wa RFI wauawa Mali
BAMAKO, Mali
WAANDISHI wa
habari wawili wa Redio France International (RFI) wameuawa siku juzi muda mfupi
baada ya kutekwa na watu waliojihami kwa silaha kaskazini mwa nchini hapa.
Wanahabari
hao waliotambuliwa kwa jina la Ghislane Dupont na Claude Verlon wameuawa muda
mfupi baada ya kumaliza mahojiano yao na msemaji wa kundi la MNLA, Ambery Ag
Rissa.
Kwa mujibu
wa Ag Rissa, waandishi hao walikamatwa mbele ya nyumba yake na watu
wasiofahamika na aligundua baada ya kusikia kelele lakini alipojaribu kutoka
nje alitishiwa na kutakiwa kubaki kimya kisha gari la watekaji kuondoka na
wanahabari hao ambao baadaye walionekana wakiwa wameuawa kwa kupigwa risasi
katika barabara ya Tinessako nje kidogo ya mji wa Kidal.
Wizara ya
mambo ya nje ya Ufaransa imethibitisha vifo hivyo na Rais Francois Hollande
ameitisha mkutano wa dharura wa mawaziri kuzungumzia suala hilo.
Bado
haijafamika chanzo cha mauaji hayo ingawa kikao cha dharura kinatarajiwa
kuzungumzia iwapo tukio hilo lina uhusiano na hatua ya Ufaransa kupeleka
majeshi yao kupambana na makundi ya wapiganaji huko Kaskazini mwa Mali tangu
mwanzoni mwa mwaka huu.
Tayari Rais
Hollande amezungumza kwa njia ya simu na Rais wa Mali Ibrahim Boubacar Keita
kuhusiana na tukio hilo ambali limekuja siku chache baada ya raia wanne wa
Ufaransa waliokuwa wakishikiliwa kama mateka nchini Niger tangu mwaka 2010
kuachiwa huru na kurejea nchini mwao.
Ghislane
Dupont alifariki akiwa na miaka 57, enzi za uhai wake alikuwa mwanahabari wa
kike akiandika zaidi habari za Afrika tangu alipojiunga na RFI mwaka 1986, amesharipoti
habari katika mataifa ya Ethiopia, Sudan kwa miaka 10 akiwa mwakilishi wa RFI
nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC.
RFI imesema Claude
Verlon (55) alijiunga nao tangu mwaka 1982 na alikuwa akitumika kwa baadhi ya
nyakati kuripoti matukio toka katika maeneo yenye migogoro duniani.
0 comments:
Post a Comment