Marekani: Boko
Haram, Ansaru ni magaidi
LAGOS,
Nigeria
SERIKALI ya
Marekani imeyataja makundi ya wapiganji wa kiislam ya nchini hapa ya Boko Haram
na lile la Ansaru katika orodha yake ya ugaidi.
Kutokana na
sheria za Marekani sasa itakuwa kosa la jinai kutoa msaada wowote kwa makundi
hayo yanayotuhumiwa kusababisha vifo vya watu wengi nchini Nigeria.
Marekani
imesisitiza kuwa hii ni hatua muhimu katika kuisaidia Nigeria na mashambulizi
kutoka katika makundi hayo mawali na kwamba sasa yatambulike kama makundi ya
kigaid kama ilivyo kwa lile la Al Qaeda.
Kutokana na
hatua hiyo ya Marekani idara zake zinapaswa kusitisha biashara zote
zinazoendesha mtandao huo wa kigaidi na kudhibiti usafirishaji wa fedha ndani
ya makundi hayo.
Pamoja na
kundi hilo kuwepo zaidi nchini Nigeria lakini Marekani inasema limekuwa
likishirikiana na mtandao wa kimataifa wa Ugaidi wa Al Qaeda ambapo matawi yake
yapo pia Afrika Magharibi na Mali.
Kundi hili
la Boko Haram lilianzishwa mwaka 2009 huku mashambulizi yake yakielekezwa
katika vituo vya jeshi,katika shule na kuendesha mapigano na vikosi vya ulinzi
nchini Nigeria.
Wachambuzi wa masuala ya kigaidi wanasema kuwa tamko hilo haliwezi kuwa mwarubaini wa kulinyong’onyeza kundi hilo kifedha kwa sababu wao hawapo nchini Marekani na wamekuwa wakipata fedha kwa kupitia njia ya kuteka nyara.
Wachambuzi wa masuala ya kigaidi wanasema kuwa tamko hilo haliwezi kuwa mwarubaini wa kulinyong’onyeza kundi hilo kifedha kwa sababu wao hawapo nchini Marekani na wamekuwa wakipata fedha kwa kupitia njia ya kuteka nyara.
REUTERS
Mwisho.
300 wahofiwa
kufariki Somalia
MOGADISHU, Somalia
WATU 300
wanahofiwa kufariki dunia katika eneo ya kaskazini mashariki mwa Somalia la
Putland kutokana na kimbunga kikali na mvua kubwa iliyonyesha katika siku
kadhaa kwenye eneo hilo.
Serikali ya
Somalia imetangaza kuwa mvua kubwa, kimbunga kikali na mafuriko vimesababisha
hali ya hatari na kwamba watu 300 wanahofiwa kuwa wamepoteza maisha na mamia
hawajulikani waliko.
Japokuwa
takwimu hizo hazijathibitishwa na chombo cha kujitegemea lakini wataalamu wa
masuala ya hewa wa Shirika la Chakula la Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO)
wanasema kuwa, mafuriko yalikuwa makubwa katika maeneo hayo ya kaskazini
mashariki mwa Somalia.
Majuzi Rais
wa Mamlaka ya Ndani ya Puntland Abdirahman Mohamud Farole aliiomba jamii ya
kimataifa kutuma misaada ya dharura kwa watu walioathika wa eneo hilo.
0 comments:
Post a Comment