Social Icons

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Thursday, December 5, 2013

Biden: China, Marekani tanueni ushirikiano

HONGKONG, China
MAKAMU wa Rais wa Marekani, Joe Biden, amezitaka China na Marekani ziimarishe na kutanua ushirikiano kwa kivitendo wenye kuonesha matokeo chanya.
biden akikagua gwaride nchini China
Pamoja na kusisitiza kutanuka kwa ushirikiano lakini alikosoa mfumo wa elimu na utawala unaotumiwa na nchi ya China.
Ziara ya Biden iliyokuwa ya ghafla katika ubalozi wa Marekani nchini China, ilikuwa na madhumuni ya kutafuta uungwaji mkono wa mpango wa Marekani wa kupunguza vikwazo kwa Wachina wanaotaka kuingia Marekani.
Biden ameliambia kundi la watu hao ambao wengi ni vijana, kwamba anatarajia wakati wa kutembelea Marekani umefika ambako watapata fursa ya kujifunza kwamba uvumbuzi unakuja pindi mtu anapopumua kwa uhuru.
"Nchini Marekani, watoto wanazawadiwa kwa kuupa changamoto mfumo uliopo na sio kuadhibiwa, na njia pekee ya kupata kipya ni kuondoa cha zamani." Biden aliwaambia vijana hao.
Kauli kama hii inayouokosoa mfumo wa utawala na kielimu wa China iliwahi kuzua mzozo baina ya nchi hizo mbili Mei mwaka huu, baada ya  Biden kuwaeleza wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Pennsylvania kwamba huwezi kufikiri tofauti katika taifa ambalo huwezi kuvuta hewa kwa uhuru, kauli iliyowaudhi wanafunzi wa chuo hicho na kusema wametukanwa na hivyo kuomba waombwe radhi.

Katika ziara yake Biden alipata wasaa wa kukutana na Makamu wa Rais wa China, Li Yuanchao, kwenye jengo la Ukumbi wa Watu wa China, ambapo alisifia jitihada za Rais Xi katika kutatua tofauti zilizopo baina ya Marekani na China. 

0 comments:

 

Sample text

Sample Text

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sample Text