Social Icons

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sunday, December 22, 2013



Obama avionya vikosi vya uasi Sudani Kusini

JUBA, Sudan Kusini
RAIS wa Marekani Barack Obama juzi amevionya vikosi vya waasi nchini Sudan Kusini vinavyofanya mapinduzi ya kijeshi baada ya kuwajeruhi wanajeshi wanne wa Marekani.
Hayo yamebainishwa kwenye taarifa kutoka ya Ikulu ya nchi hiyo imeeleza kuwa juhudi zozote za kunyakua madaraka kwa nguvu za kijeshi zitakazosababisha kukoma kwa msaada wa muda mrefu kutoka Marekani na Jumuiya ya kimataifa.
Rais Obama amesisitiza kuwa viongozi wa Sudan Kusini wanalo jukumu la kusaidia juhudi za Marekani kuwaokoa wamarekani na raia wengine huko Juba na Bor mji ambao unashikiliwa na waasi.
Onyo la rais Obama linatolewa baada ya ndege tatu za Marekani kushambuliwa kwa risasi wakati zikielekea Bor kusaidia juhudi za kuwaondoa Wamarekani nchini Sudani Kusini kutokana na kuchachamaa kwa mapigano baina ya serikali na waasi.
Jeshi la Serikali ya Sudan Kusini lipo kwenye harakati za kutaka kuukomboa mji wa Bor, ulioko kaskazini mwa mji mkuu Juba, kutoka wanajeshi walioasi na kumuunga mkono makamu wa rais wa zamani, Riek Machar aliyefukuzwa kazi hivi karibuni na rais wa nchini humo, Silva Kiir.
Baada ya kutangazwa kutekwa kwa mji huo mara moja, Marekani ilipeleka wanajeshi wake 45 kuwalinda raia wake wanaofanyashughuli zao hapo na mali zao.
Kuna taarifa zinasema kuwa ndege za Uganda pia zimekuwa zikihusika katika kusaidia serikali ya Sudan kuukomboa mji wa Bor kutoka kwa wanajeshi walioasi.
Wakati hayo yakijili kiongozi wa waasi wa Sudan Kusini Riek Machar amesema kuwa, vikosi vyake vimefanikiwa kuchukua udhibiti wa jimbo muhimu la uzalishaji mafuta la Unity nchini humo.
Makamu huyo wa zamani wa rais amedai kuwa, vikosi vyake ambavyo vinapambana na askari wa serikali vinadhibiti sehemu kubwa ya nchi hiyo. Kabla ya hapo pia jeshi la Sudan Kusini lilikuwa limetangaza habari ya kujiengua serikalini kwa Jenerali James Kwang Chol aliyekuwa kiongozi wa kijeshi katika jimbo hilo la Unity nchini humo na kujiunga na waasi.
Habari kutoka Addis Ababa, Ethiopia zinasema kuwa, ripoti iliyotolewa na Umoja wa Mataifa zinasema kuwa AU imelaani vikali mauaji dhidi ya askari wa kulinda amani wa UN na raia wasio na hatia, yaliyotekelezwa katika kambi ya nchini hapa.
Mapigano hayo yalizuka siku ya Jumapili iliyopita mjini Juba, ambao ni mji mkuu wa Sudan Kusini na hatimaye kuenea katika maeneo mengine ya nchi hiyo.

0 comments:

 

Sample text

Sample Text

PATA HABARI NA BURUDANI MBALI MBALI POPOTE ULIPO!

Sample Text